makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Disemba, 2009
Twita Kutoka Beirut: Siku ya Pili ya Warsha ya Wanablogu wa Uarabuni
Siku ya pili ya Warsha ya Wanablogu wa Kiarabu ilianza na mada inayohusu Mtandao wa Herdict, tovuti inayotumia vyanzo vya watumiaji kukusanya taarifa za uchujaji wa habari kwenye intaneti kutoka kwa watumiaji duniani kote. Mshiriki wa warsha kutoka Qatar Muhammad Basheer alituma picha kutoka kwenye mada hiyo katika ujumbe wa...
Guinea: Jaribio la Kumuua Kiongozi wa Kijeshi Dadis Camara
Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari, Kapteni Dadis Camara, kiongozi wa kikundi cha jeshi kilitwaa madaraka nchini Guinea mwezi Disemba 2008, alipigwa risasi na kujeruhiwa na mmoja wa wasaidizi wake jana mjini Conakry. Wasomaji wengi wa RFI wanaodai kuwa Camara anawajibika kwa mauaji ya waandamanaji wa upinzani yaliyotokea tarehe 28 Septemba, wanaoana kuwa haki imetendeka.
Mchakato wa Amani Nepal Unayumba
Mchakato nyeti wa kuleta amani nchini Nepal unasitasita katikati ya mapambano yanayozidi kuongezeka kati ya watu wa kundi la ki-Mao na serikali. Kundi la ki_Mao linatishia kuitisha mgomo usio na kikomo kama madai yao hayatatekelezwa.
Urusi: Jinsi Abiria wa “Nevsky Express” Walivyoeleza Habari Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Kijamii
Ajali ya treni la "Nevsky Express" ilitokea mbali na makazi ya watu. Ilichukua masaa kadhaa kwa wanahabari kufika kwenye eneo. Na hapo ndio picha na video za kwanza zilipoanza kuonekana kila mahali. je nini kilichotokea kwenye upashanaji habari wa kiraia ambao uliongoza njia ya kupashana habari wakati wa ajali ya ndege huko Urusi mwaka mmoja uliopita?