j nambiza tungaraza · Disemba, 2009

makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Disemba, 2009

China na Iran: #CN4Iran

  28 Disemba 2009

Jana, maelfu ya Wa-Irani waliingia mitaani ili kupinga dhidi ya utawala wa kiimla. Maandamano hayo yaliwakumbusha watu wa China juu ya vuguvugu la demokrasi la Tiananmen la 1989 na watumiaji wa Ki-China wa twita wanatumia alama ya #cn4iran ili kuonyesha mshikamano na wenzao wa Irani.

Singapore: Kampeni ya “Kataa Ubakaji”

  23 Disemba 2009

Nchini Singapore, mara nyingi kumbaka mke wako hakuchukuliwi kama tendo la kubaka. Waandaji wa kampeni ya “Kataa Ubakaji” wanataka kukomesha sheria inayokinga ubakaji ndani ya ndoa kwa kuzindua kampeni ya kukusanya saini ambazo zitawasilishwa kwa watunga sera. Wengi wa raia wa mtandaoni wanaiunga mkono kampeni hii.

Misitu ya Madagascar Inateketezwa kwa $460,000 kwa Siku

Wakati mataifa ya dunia yanakutana huko Copenhagen kwa ajili ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi, Madagascar, ambayo imekwishapoteza 90% ya misitu yake ya asili, inakabiliwa na tishio la biashara ya magendo ya magogo, inayotishia kuharibu kile kilichobakia katika moja ya mifumo ya mazingira yenye viumbe na mimea mingi inayotofautiana.

Ethiopia: Meles Zenawi aisaliti Afrika

Lucas Liganga aandika kuhusu usaliti wa Waziri Mkuu wa Ethiopia: “kwa bahati mbaya, Waziri Mkuu wa Ethiopia meles Zenawi ambaye ni msemaji wa Afrika kuhusu mabadiliko ya tabianchi amejiunga na Ufaransa na kubadili nakala ya Afrika, jambo ambalo limewastua wajumbe wa Afrika.”

Poland: Blogu Zataka Malipo

  16 Disemba 2009

Wasomaji wa blogu zinayoongoza za lugha ya Kipolish ni lazima wameshangazwa kuona kivinjari skrini mpya ya ukaribisho kwenye moja ya tovuti zinazopendwa: Imetangaza kwamba, kuanzia Disemba 14, 2009, kupatikana kwa blogu hiyo hakuta kuwa bila ya gharama. Jakub Gornicki anaandika kuhusu habari hiyo.

Barbados, Trinidad & Tobago:Plastiki na Uchafuzi wa Mazingira

  15 Disemba 2009

“Fanya matembezi kwenye pwani yoyote nchini Barbados – na utaona uchafu wa plastiki uliosukumwa ufukweni”: Barbados Free Press anauliza kama uuzaji wa chupa za plastiki za maji uwekewe vikwazo, wakati Mtrinidadi Keith Francis pia anaguswa na suala la uchafuzi wa mazingira kwa plastiki ulimwenguni.