Habari kuhusu Urusi

Urusi: Wapinzani Wapumbazwa na Uchaguzi wa Awali, Wapoteza Uchaguzi Halisi

RuNet Echo  30 Aprili 2013

Mwezi Agosti (mwaka 2012), Mtandao wa Sauti za Dunia uliripoti habari za wanaharakati kadhaa wanaohusika na vuguvugu la maandamano nchini Urusi wanaogombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa. Walitumaini itakuwa rahisi kushinda uchaguzi huo mdogo, ambao ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita. Oktoba 14, 2012 huku idadi ya ndogo ya wapiga kura wakiojitokeza tena ndani ya madai ya siku nyingi ya wizi wa kura katika uchaguzi, Warusi walishiriki kwa maelfu katika uchaguzi nchini kote, kupiga kura kuwachagua mameya wa miji, madiwani, na wabunge wa mikoa.

Asasi za Kiraia za Urusi “Zakaguliwa” na Mwendesha Mashitaka

RuNet Echo  15 Aprili 2013

Wanaharakati wa DemVybor katika jiji kuu la eneo la Voronezh waliripoti kwenye blogu ya DemVybor[ru] kwamba Asasi Zisizo ki-Serikali zinakaguliwa na ofisi ya mwendesha mashitaka wa umma wa jiji hilo. Mashirika manne yaliyolengwa ni wanachama wa Baraza la Haki za Binadamu la Voronezh [ru]: ni Vuguvugu la Haki za Binadmau linaloendeshwa na...

Wakati Papa Anajiuzulu, Warusi Wajiuzulu kwa Putin

RuNet Echo  12 Februari 2013

Pasipokutaka kujua matokeo ya kujiuzulu kwa Papa Benedict na athari yake kwa imani ya Kikatoliki au tafsiri ya hatua hiyo kufuatia kashfa ya udhalilishaji iliyowakabili kwa watawa, RuNet walioweka habari hiyo kwenye safu za vichekesho.

Urusi: Mlipuko Katika Kiwanja cha Ndege cha Domodedovo

RuNet Echo  25 Januari 2011

Bomu lililipuka katika kiwanja cha ndege cha Domodedovo mjini Moscow, kwa uchache vifo vya kadri ya watu kumi vimeripotiwa. Mmiminiko wa Twita unapatikana hapa (RUS) na hapa (RUS, ENG). @ann_mint, ambaye anafanya kazi Domodedovo, alikuwa ni mmoja wa watumiaji wa kwanza wa Twita kuripoti juu ya mlipuko huo; “Kuna wahanga...

Urusi: Wanablogu wakutana na Balozi wa Irani, waepa kuhoji masuala nyeti

Mkutano kati ya wanablogu wanaoongoza nchini Urusi na Balozi wa Irani jijini Moscow, siku tatu tu baada ya mwanablogu Hossein Derakshan kuhukumiwa kifungo cha miaka 19.5 jela kwa kile kilichoelezwa kuwa ni "kufanya propaganda zinazoipinga serikali" ulizionyesha wazi juhudi zisizoeleweka za diplomasia ya mtandaoni ya Irani nchini Urusi. Vilevile ulionyesha jinsi maslahi binafsi ya kibiashara pamoja na mtizamo taharuki uliopita kiasi wa baadhi ya wanablogu maarufu wa Urusi.

Urusi: Habari za Mwanzo za Milipuko ya Mabomu

RuNet Echo  9 Aprili 2010

Utaratibu wa Jumatatu asubuhi mjini Moscow ulivunjwa leo na milipuko ya mabomu mawili mabomu ya kujiua, ambayo yaliua watu wapatao 38 na kujeruhi kwa uchache watu wapatao 70. Alexey Sidorenko anatafsiri baadhi ya taarifa za mwanzo kutoka katika ulimwengu blogu za Urusi.