· Oktoba, 2012

Habari kuhusu Mazingira kutoka Oktoba, 2012

India: Mgogoro wa Mtambo wa Nyuklia wa Kudankulam Waendelea.

  22 Oktoba 2012

Mradi wa Nguvu za Nyuklia mjini Koodankulam katika wilaya ya Tirunelveli iliyo katika Jimbo la kusini la Tamil Nadu nchini India umeanza kufanya kazi mwezi uliopita lakini maandamano ya kuupinga mradi huo umeendelea na kamata kamata inasababisha waandamanaji kuishia jela. Juma hili limeshuhudia maandamano yakienea India yote kwa ushirikiano na watu wanaopinga matumizi ya Mtambo wa Nyuklia.

Zambia: Filamu yaYouTube Kuhusu Athari za Machimbo ya Madini

Filamu ya Uchunguzi yenye jina "Zambia: Shaba Nzuri, Shaba Mbaya" inayohusu machimbo ya shaba nchini Zambia na athari zake kwa jamii imewekwa kwenye mtandao wa YouTube na mpaka sasa imevuta watazamaji zaidi ya 6,000. Baada ya kuitazama filamu hiyo, mtumiaji mmoja wa mtandao wa YouTube aliandika, "Jililie eeh nchi yangu nzuriKwa nini tubaki masikini katikati ya utajiri huu wa madini yanayochimbwa kwa gharama ya afya za wenyeji?"