Kuna taarifa zisizodhibitishwa zinazosema kwamba vikosi vya pamoja vya Kisaudi, ambavyo vimekuwa vikiishambulia Yemen kwa mabomu kwa zaidi ya miezi miwili sasa vimelilenga Bwawa la Marib, moja wapo ya maajabu makuu ya katika ulimwengu wa ubunifu wa kale wa kiufundi.
Kwenye mtandao wa Twita, Hussain Albukhaiti anadai:
Unconfirmed reports: #Saudi Jets has Just targeted the historic #Marib Dam NW #Yemen
http://t.co/rZYWUF2Qe6 pic.twitter.com/XTqHrXMGAk
— Hussain Albukhaiti (@HussainBukhaiti) May 30, 2015
Taarifa zisizothibitishwa: Ndege za kijeshi zimeshambulia bwawa la Mariba
Akijibu twiti hiyo, Albukhaiti anaweka picha za bwawa hilo linalokadiriwa kujengwa katika karne ya nane kabla ya Kristo na linasemekana kuwa bwawa la zamani zaidi duniani:
Marib Dam NE #Yemen dating from 8th century BCE was targeted yest by #Saudi jet Prev Tweet https://t.co/c746huac1P pic.twitter.com/D8nj6yA5M1
— Hussain Albukhaiti (@HussainBukhaiti) May 31, 2015
Uharibifu wa Bwawa la Mariba limejengwa karne ya nane (KK) na limelengwa na ndege za kijeshi za Kisaudi
Kiwango cha uharibifu wa miundo mbinu na historia ya Yemeni bado hakijajulikana. Tunaendelea kukusanya taarifa na vyanzo zaidi viko hapa kuhusu tukio hilo kwenye dawati la Global Voices Uthibitisho, mradi unaowezeshwa kwa ushirikiano na Meedan Checkdesk, zana ya mtandaoni ya uthibitisho wa habari, pamoja na Global Voices Online.
Unaweza kuacha maoni yako hapa kuchangia dondoo kuhusu habari hii au hata kuungana na timu yetu ya habari.