Nini Tofauti ya Kusoma na Kuelimika?

Pedro Muller anatafakari kuhusu matatizo yanayoukabili mfumo wa shule, taasisi anayosema ilimaanisha mazingira tofauti ya kihistoria. Kwa kusema hayo, anabainisha umuhimu wa dhana hizi mbili zinazofanana lakini zikimaanisha nyakati mbili tofauti: “Kusoma” na “kuelimika”:

El educar se va más allá de memorizarse un par de nombres y olvidarlos al siguiente día, consiste en aprender tener la curiosidad de preguntarse qué hay detrás de lo obvio, es adquirir habilidades, ejercitar tu pensamiento lateral un pensamiento divergente o como muchos dicen “fuera de la caja”, educarse también es crear y hacer convertir nada en algo, innovar.

Nosotros aprendemos mejor en grupo es parte de nuestra naturaleza, discutir, pensar y reflexionar sobre un tema en específico sacar conclusiones, como muchos dicen la mejor manera de educarse es aprender.

TKuelimika kunaenda mbali zaidi ya kukariri majina kadhaa na kuyasahau siku inayofuata. Kuelimika ni kuwa na udadisi na kuhoji yale yaliyofichika nyuma ya kinachoonekana kuwa mazoea, ni kuwa na ujuzi, kuutumia uwezo wa kufikiri tofauti, fikra mbadala tunazoweza kuziita “kufikiri nje ya boksi”. Kuelimika ni kujifunza kuwa mbunifu na mgunduzi.

Tunajifunza vizuri kwenye makundi; ni sehemu ya asili yetu kujadili, kufikiri na kutafakari mada mahususi na kufanya mahitimisho. Inasemekana kwamba namna nzuri ya kuelimika ni kujifunza.

Muller anawakaribisha wasomaji wake kutazama video ifuatayo iliyo katika Kiingereza, ambako Logan LaPlante anazungumzia dhana ya “kuidua elimu” au “dukuaelimu”, anayosema ni mchakato wa kujifunza kwa kikundi, kwa mtindo wa kujaribu na, zaidi, umuhimu wa ubunifu.

Endelea kusoma makala ya Muller hapa, au mfuatilie kwenye mtandao wa Twita.

Makala haya ni sehemu ya 46 ya #LunesDeBlogsGV (JUmatatu ya blogu ya GV) mnamo Machi 23, 2015.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.