
Wanawake 12 walifanya maandamano ya kupinga kombe la dunia tarehe 7 Julai jijini Shanghai. Picha na Weibo Offbeat China.
Offbeat China alieleza kwa nini wanawake hao wana hasira na jinsi Kombe la Dunia linavyoharibu mahusiano ya kifamilia nchini China.
Wanapinga mambo mawili makubwa: 1) wapenzi wao kupuuza majukumu yao ya kifamilia kwa sababu ya kuangalia mpira usiku wa manane; 2) tabia za kucheza kamari kwa mashindano hayo.