makala mpya zaidi zilizoandikwa na mdoti
Lebanoni: Utawala wa Dinosauri
Punde baada ya matukio ya unyanyasaji ya hivi karibuni nchini Lebanon, Msemo wa “Utawala wa Dinosauri” ulianza kutumika na wanaharakati wa mtandaoni kwenye kampeni dhidi ya uvamizi wa namna hii katika mitandao yao. Mwanablogu wa Lebanon Tony anaeleza maana ya msemo huo.
Brazil: Ukatili Dhidi ya Wanawake Kila Siku
Nchini Brazil, wanawake 10 huuwawa kila siku. Mauaji ya hivi karibuni na anasadikiwa kuwa mzazi wa mtoto wake, mlinda mlango nyota aneyetarajiwa, yamewasha cheche za majadiliano katika uwanja wa blogu kuhusu ukatili dhidi ya wanawake.
Asia ya Kusini Mashariki : Ngono na Udhibiti wa Mtandao
Uratibu wa maudhui katika intaneti unaonekana kana kwamba ni kinyume na demokrasia lakini serikali za Kusini Mashariki mwa Asia zinaweza kuhalalisha kitendo hicho kwa kuzusha haja ya kuwaokoa vijana kutoka kwenye janga la tabia za ngono holela.
Irani: Je Blogu Zimepoteza Umaarufu Tangu Uchaguzi
Je uchaguzi wa rais ulibadili jinsi nyenzo za uanahabari wa kiraia zinavyofanya kazi nchini Irani? Wanablog wa Irani kumi na moja na wandishi wa habari wanaowakilisha sehemu tofauti za misimamo ya kisiasa wamejibu dodoso kuhusu mabadiliko uanahabari wa kiraia nchini Irani tangu Uchaguzi.
Colombia: Mockus na Fajardo Waungana kwa Ajili ya Uchaguzi wa Rais
Mameya wawili wa zamani wa amajiji 2 makubwa zaidi nchini Kolombia wameunganisha majeshi kugombea katika uchaguzi wa rais wa Mei 30 kwa tiketi moja. Umoja huu mpya wa Chama cha Kijani umepokewa vizuri na watumiaji wa vyombo vya habari vya kijamii, ambo ni sehemu kubwa ya mkakati wa kampeni.
Guatemala: Hadithi ya Maziwa Mawili, Macaws na Malkia
Wanaharakati wa mazingira wana hofu kuhusu kuendelea kuchimbwa mafuta katika Hifadhi ya taifa ya Laguna del Tigre, ambayo ni moja ya maziwa ya asili nchini guatemala ambalo lina utafuti wa mazingira na ambalo liko hatarini.
Piga kura kuchagua “Blogu Bora Zaidi”
Upigaji kura mtandaoni umeanza kwa ajili ya Tuzo ya Blogu Bora Zaidi inayotolewa na Deutsche Welle (Shirika la Habari la Ujerumani), moja kati ya mashindano ya blogu yenye hadhi kubwa kimataifa na blogu zilizotajwa kushiriki ni za lugha kumi na moja tofauti. Unaweza kuipigia kura blogu uipendayo hadi April 14, 2010.
South Africa: Mauaji ya kiongozi wa Afrikaner Resistance Movement
Usiku wa Tarehe 3, Aprili 2010, kiongozi wa kundi la watetezi wa Waafrika Kusini wenye asili ya Udachi (Afrikaans Weerstandsbeweging (AWB), au Afrikaner Resistance Movement), Eugene Terre'Blanche, aliuawa. Je raia wa dijitali wana nini cha kusema kuhusu kifo chake na mustakabali wa mahusiano baina ya watu wa rangi tofauti nchini Afrika kusini?
Nchi za Balkani: Ufanano Baina ya Facebook na Chama cha Kikomunisti cha Yugoslavia
Filip Stojanovski anatafsiri orodha ya vitu vinavyofanan kati ya Facebook na Chama cha kikomunisti cha Yugoslavia (CPY).
Indonesia: Sony yamkabili Sony
Sony AK wa Indonesia alitishiwa kushitakiwa kwa kukiuka sheria za matumiza ya nembo na shirika la Sony la Japan kama hatafunga tovuti yake binafsi yenye jina www.sony-ak.com. Suala hili lilizua mwitiko mkali katika jamii ya wanamtandao na kuilazimisha kampuni ya Sony kutupilia mbali shauri hilo.