makala mpya zaidi zilizoandikwa na mdoti kutoka Aprili, 2010
Irani: Je Blogu Zimepoteza Umaarufu Tangu Uchaguzi
Je uchaguzi wa rais ulibadili jinsi nyenzo za uanahabari wa kiraia zinavyofanya kazi nchini Irani? Wanablog wa Irani kumi na moja na wandishi wa habari wanaowakilisha sehemu tofauti za misimamo ya kisiasa wamejibu dodoso kuhusu mabadiliko uanahabari wa kiraia nchini Irani tangu Uchaguzi.
Colombia: Mockus na Fajardo Waungana kwa Ajili ya Uchaguzi wa Rais
Mameya wawili wa zamani wa amajiji 2 makubwa zaidi nchini Kolombia wameunganisha majeshi kugombea katika uchaguzi wa rais wa Mei 30 kwa tiketi moja. Umoja huu mpya wa Chama cha Kijani umepokewa vizuri na watumiaji wa vyombo vya habari vya kijamii, ambo ni sehemu kubwa ya mkakati wa kampeni.
Guatemala: Hadithi ya Maziwa Mawili, Macaws na Malkia
Wanaharakati wa mazingira wana hofu kuhusu kuendelea kuchimbwa mafuta katika Hifadhi ya taifa ya Laguna del Tigre, ambayo ni moja ya maziwa ya asili nchini guatemala ambalo lina utafuti wa mazingira na ambalo liko hatarini.
Piga kura kuchagua “Blogu Bora Zaidi”
Upigaji kura mtandaoni umeanza kwa ajili ya Tuzo ya Blogu Bora Zaidi inayotolewa na Deutsche Welle (Shirika la Habari la Ujerumani), moja kati ya mashindano ya blogu yenye hadhi kubwa kimataifa na blogu zilizotajwa kushiriki ni za lugha kumi na moja tofauti. Unaweza kuipigia kura blogu uipendayo hadi April 14, 2010.
South Africa: Mauaji ya kiongozi wa Afrikaner Resistance Movement
Usiku wa Tarehe 3, Aprili 2010, kiongozi wa kundi la watetezi wa Waafrika Kusini wenye asili ya Udachi (Afrikaans Weerstandsbeweging (AWB), au Afrikaner Resistance Movement), Eugene Terre'Blanche, aliuawa. Je raia wa dijitali wana nini cha kusema kuhusu kifo chake na mustakabali wa mahusiano baina ya watu wa rangi tofauti nchini Afrika kusini?
Nchi za Balkani: Ufanano Baina ya Facebook na Chama cha Kikomunisti cha Yugoslavia
Filip Stojanovski anatafsiri orodha ya vitu vinavyofanan kati ya Facebook na Chama cha kikomunisti cha Yugoslavia (CPY).
Indonesia: Sony yamkabili Sony
Sony AK wa Indonesia alitishiwa kushitakiwa kwa kukiuka sheria za matumiza ya nembo na shirika la Sony la Japan kama hatafunga tovuti yake binafsi yenye jina www.sony-ak.com. Suala hili lilizua mwitiko mkali katika jamii ya wanamtandao na kuilazimisha kampuni ya Sony kutupilia mbali shauri hilo.
Muziki Wenye Ujumbe – Video Mpya za Muziki Kutoka Tibet
Mradi wa kutafsiri Blogu uitwao High Peaks Pure Earth hivi karibuni umetupia jicho “muziki wenye ujumbe” kwa kutafsiri mashairi ya nyimbo za Tibet kutoka video za Muziki zilizowekwa kwenye mtandao. Tarehe 10 Machi mwaka huu , blogu hiyo iliweka video ya hip hop inayoitwa “New Generation” (“Kizazi kipya” kwa Kiswahili)...
Tunisia: Wanablogu wa Tunisia Wazungumza Kiingereza
Wanablogu wa Tunisia walizoea kuepuka kutumia Kiingereza (lugha ya tatu nchini mwao), na badala yake waliandika kwa Kiarabu (na wakati mwingine kwa lahaja za Tunisia) au Kifaransa. Lina Ben Mhenni anazitupia macho baadhi ya blogu zinazoandikwa kwa lugha ya Kiingereza.