Kwa mara ya pili ndani ya kipindi cha miezi minne tu, mwandishi wa habari wa Venezuela na mwanaharakati, Luis Luis Carlos Díaz, amenyanyaswa kupitia akaunti yake ya Twita na simu yake ya mkononi na kikundi kinachojulikana kama “wezi wa akaunti za mtandaoni”, na ambao hutumia jina la N33, na bila shaka ni kundi lilelile la watu ambao miezi michache iliyopita liliiba maneno ya siri ya akaunti za Twita na baruapepe ya karibu watu thelathini maarufu wa Venezuela, baadhi yao ni waandishi wa habari Sebastiana Barráez, Ibéyise Pacheco, mchekeshaji wa kisiasa Laureano Márquez, mwanaharakati Rocío San Miguel na mwandishi Leonardo Padrón, miongoni mwa wengine wengi. Kundi hili linajihusisha na watu wasiojulikana wanaojitapa kuwa waungaji mkono wa Rais Hugo Chávez.
Mwezi Desemba, watu maarufu kadhaa walitoa taarifa [es] kwa marais waliokuwa jijini Caracas ili kushiriki kwenye Mkutano wa CELAC ulioitishwa na Rais wa Venezuela Hugo Chávez:
Las cuentas de venezolanos con visiones críticas ante las políticas del gobierno, ubicados en distintos campos como el periodismo, la economía, la vida universitaria, los derechos humanos, la cultura y la justicia, entre otros, han sido “hackeadas” por individuos que asumen esa tarea agresora como un mecanismo de defensa del proceso político impulsado por el presidente Hugo Chávez.
Iria Puyosa (@NSC) alituma ujumbe wa Twita unaoonyesha uso wa akaunti ya Twita ambapo udhalimu huo umekuwa ukiibukia:
Díaz, ambaye licha ya kuwa mwanaharakati wa haki za binadamu na mchangiaji katika GV, vilevile anafanya kazi kama Mratibu wa Mawasiliano na Mitandao katika Kituo cha Gumilla, ambacho kinashughulika na utafiti na harakati za kijamii kinachoongozwa na Shirika la Wajesuiti nchini Venezuela.
Kwenye Twita, watu wameandika maoni ya kupinga unyanyasaji anaofanyiwa Luis Carlos:
@Jogreg: @N33DOS està acosando telefonicamente al pana @LuisCarlos. Ya basta!
@NSC: Parapolicías le ofrecen “trato VIP” a @LuisCarlos http://bit.ly/x9jvIL Si se equivocan x allí la respuesta también será VIP y global.
@acianela: El inaceptable acoso a @LuisCarlos RT @IPYS Venezuela: Periodista y ciberactivista es amenazado telefónicamente
Luis Carlos Díaz aliwahi kuandika kuhusu matukio kama haya siku za nyuma. Kupitia makala yake [es], ya mwezi Septemba, 2011 alisema:
La acción dejó de ser una travesura cuando el grupo N33 emitió un comunicado, leído en el canal del Estado, VTV, en el que “aclaraban” que accionaron por razones políticas en contra de cuentas que criticaban al presidente de la República y por lo tanto cualquier opositor con visibilidad mediática estaría en la mira.
Imeelezwa kwamba, kundi hilo hata limejiita “wezi wa akaunti za mtandaoni”, wala hawapaswi kujiita hivyo, hasa kwa kuzingatia kwamba walipata seti za mwanzo za maneno ya siri (au nywila) ya akaunti kwa kutumia mbinu kama vile uhandisi wa kijamii kwa kubuni maneno ya siri ambayo mtu angeweza kuyapata kirahisi. Hata hivyo, kwa vile wameteka nyara akaunti ya mwizi wa Venezuela wa akaunti za mtandaoni “white hat” RaFa Núñez, hivi sasa kuna mashaka kwamba huenda wanashirikiana na Shirika linalotoa huduma za intaneti ambalo linamilikiwa na serikali ya Venezuela.
Katika ujumbe kwa umma [es] ambao umerudiwarudiwa katika blogu mbalimbali za raia wa Venezuela, Luis Carlos amesema:
Nos enfrentamos a una nueva forma de ciberguerra más focalizada, de desactivar individuos sin mancharse mucho las manos, de afectar la libertad de expresión en Internet y acabar con las críticas gubernamentales. Este es una suerte de paramilitarismo digital, en el cual se buscan personas externas, e incluso espontáneos, para que eliminen gente en redes sociales.