
Radi ikipiga aridhi. Baadhi ya watoto wa Afrika wameaminishwa kuwa radi inaweza kuwapiga wakivaa nguo nyekundi. Picha ya Creative Commons iliyowekwa mtandaoni na mtumiaji wa Wikipedia, Jessie Eastland.
Alama ishara ya vichekesho, #ThingsIBelievedInAsAChild [Mambo niliyoamini Utotoni], imekuwa ikipata umaarufu nchini Afrika Kusini, ambapo watu wanaambiana imani kadhaa za kimila walizoamini enzi zao wakikua.
Hapa ni baadhi ya twiti zilizochanguliwa kwenye alama ishara hiyo.
Mtumiaji aitwaye “Divinity” ilibidi awe makini anapokula chungwa, kwa sababu:
#ThingsIBelievedInAsAChild
If you swallow an orange seed, an orange tree starts growing in your stomach— Divinity ?? (@CAN_Divine) February 17, 2017
Kama ukila mbegu za chungwa, mchungwa ungeanza kuota kwenye tumbo lako
“Big Boss” aliamini ilifaa kupiga mluzi wakati wa mchana:
#ThingsIBelievedInAsAchild
Never whistle at night, it brings bad luck.— Big Boss (@Thee_Psychic) February 17, 2017
Usipige mluzi usiku, utapata mikosi
Levi alifikiri kimo kilidumazwa na kurukwa:
If someone jumps a leg over you, you won't grow tall unless they unjump you ???#ThingsIBelievedInAsAChild
— Levi The-Truth (@Levi_Scary_T) February 17, 2017
Kama mtu angekuruka kwa mguu, hutarefuka mpaka afute mruko wake
Televisheni inafanyaje kazi?:
#thingsibelievedinasachild people who are on TV are actually inside TV pic.twitter.com/vZeZb8drqo
— Oa Matatiele (@Paballo65M) February 17, 2017
Watu wanaoonekana kwenye televisheni kimsingi wanaishi ndani ya televisheni
Ukiona gari lililobeba maiti linapita:
#ThingsIBelievedInAsAChild that if you see this car, you must hold a hair strand till it passes by???or else pic.twitter.com/obL5MiW1Kr
— noluthando (@KgabuNoluthando) February 17, 2017
Ukiona gari hili, lazima ushike nywele mpaka likupite
Ilibidi uvae “Nguo kali za Jumapili”, siku ya Jumapili:
I can only wear new clothes on a Sunday and not during the week #ThingsIBelievedInAsAchild
— Zinhle Mashiloane (@ZeeMach) February 17, 2017
Ninaweza kuvaa nguo mpya siku ya Jumapili na sio siku nyingine za wiki
“#Avantgardehipster” aliamini:
#ThingsIBelievedInAsAchild
Was told albinos don't die but they just vanishTill now i haven't seen obituary of an albino ??
— #Avantgardehipster (@1real_bill) February 17, 2017
Niliambiwa Albino hawafi bali hupotea
Mpaka sasa sijawahi kuona tangazo kuwa albino amefariki
Mtumiaji mmoja wa Twita aliweka picha ifuatayo sambamba na twiti yake:
#ThingsIBelievedInAsAChild
Eating too much will make me fit & strong. pic.twitter.com/V21ZTXhNQL— ®Azee (@TheRealAzee_RSA) February 17, 2017
Kula sana kunanifanya niwe na afya njema na mwenye nguvu
Anasemaje?:
I genuinely believed that testicles were eggs#ThingsIBelievedInAsAChild
— Zanel Ndzume (@Zanel_zn6) February 17, 2017
Niliamini kwa hakika korodani ni zilikuwa mayai
Watoto hutokea wapi?:
#ThingsIBelievedInAsAChild Babies were bought not born
— Luvuyo Mkonqo (@LMkonqo) February 17, 2017
Watoto hununuliwa hawazaliwi
Taa ya jokofu inajizimaje?:
That there was a tiny man that turned on the light in the fridge whenever i opened it. #ThingsIBelievedInAsAChild
— theREALone (@Babs_2by4) February 17, 2017
Kwamba kuna mtu mdogo anayezima taa ya jokofu kila ninapofungua mlango wake
Unawezaje kuwatambua matajiri?:
#ThingsIBelievedInAsAChild if you had this at home, you were rich people?? pic.twitter.com/XPwHRsn1rY
— #See_Yowa_Life?? (@IraguhaHerbert) February 17, 2017
Kama ulikuwa na kitu hiki nyumbani, basi wewe ni tajiri
Kama hutaki kuwa kibogoyo maisha yako yote…:
After removing a tooth, if you don't throw it on the roof you'll never grow another one to replace it #ThingsIBelievedInAsAChild
— JoyLiladzani M (@Liladzani1) February 17, 2017
Ukishang'oa jino, usipolitupia kwenye bati jino jingine halitaota badala yake
“DJASH” alifikiri:
All toothpaste are called colgate
All bleach products are Jik
All soaps are either called Lux or Sunlight!
— #SayMyNameBaby (@DJASH_214) February 17, 2017
Dawa zote za mswaki ziliitwa Colgate
Dawa zote za kutoa madoa kwenye nguo ziliitwa JIK
Sabuni zote ziliitwa ama Lux au Sunlight
Jik, Colgate, Lux na Sunlight ni bidhaa maarufu kwenye eneo la kusini mwa bara la Afrika.
Angalia utabiri wa hali ya hewa kabla hujavaa nguo nyekundu:
#ThingsIBelievedInAsAChild don't wear red if there's a thunder storm … lightning might strike you real quick
— ig: ms_yazlee (@Yazmiin_Yawlee) February 17, 2017
Usivae nguo nyekundu kama kuna radi…radi inaweza kukupiga kirahisi sana