
Mzazi wa Kisyria Wael Zain anadai mwanae wa kiume mwenye uraia wa Uingereza, mwenye miaka mitano, amekwama Syria na kwamba Ubalozi wa Uingereza haujamsaidia kukutana nae. Picha imewekwa kwenye mtandao wa Twita.
Wael Zain, Msyria anaishi na kufanya kazi jijini Londoa, ameingia kwenye mtandao wa Twita kutafuta kusikilizwa kufuatia tatizo la mwanae mwenye umri wa miaka mitano, Maudh, mwenye uraia wa Uingereza, ambaye amekwama na kubaki Syria kwa miaka mitatu.
Katika mfululizo wa twiti zake, Zain anaeleza kwamba mwanae huyo, anayedai kuwa alipigwa risasi, anaishi na mama yake kwenye kijiji fulani eneo la Deraa, na anahitaji matibabu kuokoa maisha yake. Anadai kwamba Ubalozi wa Uingereza umekuwa kiziwi kila alipofanya jitihada za kuwasilisha maombi yake.
Akiandika mwenyewe kutoka Deraa, Syria, Zain anatwiti:
Please help my 5yr old son (British) in Syria come home. @foreignoffice has abandoned him. @guardian @bbclysedoucet pic.twitter.com/VJ0ZWvYxnG
— Wael Zain (@Wael_Zain) April 20, 2014
Tafadhali msaidieni mwanangu wa miaka 5 (Mwingereza) aliyeko Syria aweze kuja nyumbani. Ubalozi wa Uingereza umemtelekeza
Anaeleza:
@bbclysedoucet with his mother in a village near Nawa in Deraa. Has been there for over 3 years. 2 weeks ago he was shot at.. He needs help
— Wael Zain (@Wael_Zain) April 20, 2014
Kwa sasa yuko na mama yake kijijini karibu na eneo la Nawa huko Seraa. Amekuwa huko kwa miaka mitatu. Wiki mbili zilizopita alipigwa risasi. Anahitaji msaada
Katika twiti nyinginezo, alizozielekeza kwa Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Ungereza William Hague, Zain anaomba:
@WilliamJHague my 5 year old British son stuck in #Syria has been abandoned by your office.
— Wael Zain (@Wael_Zain) April 19, 2014
Mhe Willian Hague mwanangu mwenye miaka mitano amekwama nchini Syria na ofisi yako imetelekeza.
Anaongeza:
The British government pledged to help vulnerable Syrian refugees mainly women + children but refuse to help a British child. @williamjhague
— Wael Zain (@Wael_Zain) April 19, 2014
Serikali ya Uingereza iliahidi kuwasaidia wakimbizi walio kwenye hatari nchini Syria hasa hasa wanawake na watoto lakini imegoma wamsaidia mtoto wa Kiingereza
Zain anasema hajamwona mwane kwa miaka mitatu na anaweka picha ya mara ya mwisho aliyonayo:
last picture I have of my son in #Syria. haven't seen him for 3 yrs. needs urgent medical treatment. @WilliamJHague pic.twitter.com/S76FoALkNO
— Wael Zain (@Wael_Zain) April 19, 2014
Hii ndiyo picha ya mwanangu akiwa Syria. Sijamwona kwa miaka mitatu. Anahitaji matibabu.