
The view over Independence Square from the roof of Globus shopping center in Kyiv, Ukraine (February 19)
Photo by Anastasia Vlasova © Copyright Demotix
Mwanafunzi jijini Kyiv, Ukraine alitwiti kuanzia alfajiri mpaka usiku wa manane wakati wa siku ya mapigano kati ya waandamanaji na polisi yalisababisha vifo zaidi ya 25 na mamia wengine wakijeruhiwa.
Siku ya leo, Februari 18, 2014, Bunge la Ukraine limeshindwa kudhibiti mamlaka ya Rais Viktor Yanukovych, mlengwa mkuu wa maandamano hayo yaliyoendelea kwa miaezi mitatu kwenye viwanja vya Maidan Nezalezhnosti.
Hapa chini ni twiti zilizochaguliwa na @Mira_mp ambaye ni shuhuda wa matukio hayo, na baadae akijitolea kuwasaidia wajeruhi hospitali.
Twiti zake za kwanza zinaonyesha sura kamili ya namna mapigano yalivyoanza:
і знову я надихаюсь цього газу.
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Inaonekana kama nitavuta hewa iliyojaa moshi wa mabomu ya kutoa machozi, kwa mara nyingine.
на Грушевського знову горять шини)
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Kwenye mtaa wa Hrushevskogo [ambako mapigano yalianzia mwezi uliopita] matairi yanachomwa tena)
в Маріїнці тітушкам кричать "раби" і показують гроші)) вони соромляться і відвертають голови #Євромайдан
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Kwenye bustani ya [Mariinsky] watu wanapiga kelele “watumwa!” kwa titushki [wahuni waliokodiwa na serikali kuwapiga na kuwadhalilisha waandamanaji] na kuwaonyesha noti)) wanakasirika na kuondoka
зараз горить намет в Маріїнці. взагалі, тут відбувається щось незрозуміле. і зв'язку практично немає
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Hema kwenye bustani ya [Mariinsky] linaungua sasa hivi. Kwa ujumla, haijulikani nini kinaendelea hapa na mtandao wa simu za mkononi unapatikana kwa shida.
Twiti zake zilizofuatia alizituma akiwa anaelekea hospitali. Muda halisi unaonyesha kwamba ilikuwa ni baada ya polisi na vikosi maalumu vya kutuliza ghasia vilipoanza kupambana na waandamanaji karibu na jengo la Bunge.
їдемо в лікарню. в 2 татових друзів серйозні травми голови і руки. ця революція стає війною.
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Tunaelekea hosptali. Marafiki wawili wa baba yangu wamejeruhiwa vibaya -mmoja kichwani na mwingine mononi. Mapinduzi haya yanageuka kuwa vita.
Kuna wasiwasi kuwa polisi wanaweza kuanza kuwakamata wale wanaotoa taarifa za majeruhi, na akatwiti:
напевно не варто їхати в лікарню. краще в аптеку, обробити рани і везти їх додому
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Labda inawabidi kutokwenda hosptali. Waishie kwenye duka la dawa, watibu majeraha yao na warudi nyumbani.
Baadae, alirudi Maidan kufuatilia matukio yanayoendelea bungeni.
тепер ми знову на Майдані. надіюсь, Бо прийде в себе, в нього поранення в голову.
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Sasa tumerudi Maidan. Ninaamini Bo amepata fahamu tena, ana jeraha kichwani.
Дивились включення з ВР. якась бабуся: "і за цих виродків голосували сусіди? сьогодні зроблю їм!" я люблю цих людей!)
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Tulikuwa tunatazama matangazo ya moja kwa moja kutoka [bungeni]. Bibi mmoja anasema: “Hawa ni wapumbavu ambao wajirani zangu waliwapigia kura? leo watakuwa kwenye matatizo!” Ninawapenda watu wa namna hii!)
На Майдані дивляться стріми. жінок та чоловіків без захисту не пропускають
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
[Watu] wanafuatilia matangazo ya Maidan. Wanawake kwa wanaume bila [kofia za kukinga kichwa na nguo nyingine za kujikinga] hawaruhusiwi kuingia.
"Рибака забрали швидкою" реакція людей- хтось знає номер швидкої? кинемо коктейлі!
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Rybak [Spika wa Bunge] amechukuliwa na gari la wagonjwa. Hasira za waandamanaji -hivi kuna anayejua gari hilo ni lipi? inabidi tusherehekee!
3 померлих. мирний наступ перейшов у війну
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Watu watatu [waliripotiwa] kuuawa. Maandamano ya amani yamegeuka kuwa vita.
Беркут стріляє і кидає каміння з глобусу #євромайдан
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Berkut [kikosi cha kutuliza gahsia] wanaturushia risasi hovyo na wanarusha mawe kutokea kwenye eneo la maduka ya Globus.
На вулиці величезна к-ть людей. метро не працює, багато людей йдуть на Майдан
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Kundi kubwa la watu wako mtaani. Treni imesimamisha huduma zake, watu wengi wanatembea kuelekea Maidan.
Через 7 хвилин буде 18.00. не перестаю захоплюватись кожним, хто залишився на Майдані! тут багато літніх людей і жінок!
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
saa 12 kasoro dakika 7 [saa ya mwisho ambayo serikali iliweka kwa waandamanaji kuondoka]. Ninajivunia bila kipimo kila mtu aliyeendelea kubaki Maidan! Kuna wazee na wanawake hapa!
Kwa jinsi polisi wa kutuliza ghasia wanavyoshambulia Maidan majeruhi kadhaa waliripotiwa maeneo yote. Waandamanaji waliwaomba wanawake na watoto kuondoka kwenye maeneo yenye ghasia.
не можу бути вдома. йду в лікарню на Шовковича
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Siwezi kukaa nyumbani. Naenda hospitali kwenye mtaa wa Shovkovycha.
не можу брехати батькам і Дену. але і не йти на Майдан також не можу. вимкнений телефон – немає запитань
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Siwezi kuwadanganya wazazi na Dan. Lakini siwezi kukaa mbali na eneo la Maidan vile vile. Zima simu na hakuna swali litaulizwa.
Twiti yake iliyofuata ilikuwa ni wakati ametoka hospitali.
лікарі нічого не кажуть про стан Бо. я не можу читати новини по тві, до того ж в мене сідає батарея. зустрінемось там
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Madaktari hawajasema lolote kuhusu hali ya Bo. Siwezi kusoma habari mpya kwenye [twita] na betri yangu imekwisha. Nitakutana navyi huko
приїхали в 17 лікарню. тут величезна кількість поранених людей! приходять кияни і забирають додому неважких потерпілих #Євромайдан
— Mira (@Mira_mp) February 18, 2014
Tumekuja hospitali chumba namba 17. Kuna idadi kubwa sna ya majeruhi hapa! Wakazi wa jiji la Kyev wamekuja na kuwachukua wale wenye majeraha madogo
багато крові і трупів.
це найстрашніша ніч в моєму житті
— Mira (@Mira_mp) February 19, 2014
Damu inatiririka na miili ya watu waliokufa imetapakaa. Huu ni usiku wa kuogofya kuliko siku zote kwenye maisha yangu.
в мене на руках помер хлопець, якому прострелили голову і живіт. цю ніч я ніколи не забуду.
— Mira (@Mira_mp) February 19, 2014
Kijana aliyepigwa risasi kichwani na tumboni amefia mkononi mwangu. Sitausahau usiku huu.
Posti hii ni sehemu ya habari zetu maalumu kuhusu Ghasia za Ukraine.
1 maoni
marekani ndiye msababishaji wa vita na kukosekana kwa amani ktk nchi mbalimbali duniani kwa maslahi yake binafsi na umwagikaji wa damu,kiufupi viongozi wa amerika wananuka damu.