Habari kuhusu Wakimbizi
Uanaharakati na Umama Barani Asia
Je, mwanamke anatoa sadaka zipi ili kupigania jambo analiamini? Je, watoto wake wanaathiriwa vipi na mateso yanayoelekezwa kwake? Makala hii inachambua kwa kifupi maisha ya wanawake wanaharakati katika Asia ambao pia ni ma-mama.
Australia: Wanawake wa Kenya wakataliwa haki ya ukimbizi
Wanawake wawili wanakabiliwa na uwezekano wa kutimuliwa kutoka Australia baada ya maombi yao ya kuomba hifadhi kukataliwa, pamoja na hatari wanayoweza kuipata ya kulazimishwa tohara ya kike ikiwa watarudishwa nyumbani.
Indonesia: Tetemeko Kubwa Laikumba Sumatra
Mji wa mwambao wa Padang, Sumatra Magharibi umeharibiwa tena na tetemeko la ardhi.
Philippines:Mafuriko Mabaya Zaidi Katika Kipindi cha Miaka 40
Kimbunga kilichopewa jina la 'Ondoy" kimeikumba Philippines jumamosi iliyopita na kusababisha mafuriko mabaya zaidi katika kipindi cha miaka 40 ambayo yamesababisha vifo vya watu 50 na kusababisha wakazi 280, 000 kupoteza makazi. Tovuti za kijamii zilipashana habari za kimbunga hicho na jinsi ya kuwasaidia walioathirika.
Sri Lanka: Wanablogu Watathmini Kifo cha Kiongozi wa LTTE
Serikali ya Sri Lanka imetangaza kwa kupitia vyombo vya habari vya taifa pamoja na ujumbe wa simu za mkononi mchana leo (Jumatatu, 18 Mei, 2009) kwamba kiongozi wa Kundi linalotaka kujitenga la Wa-Tamil, the Liberation Tigers of Tamil Eelam (LTTE), Vellupillai Prabhakaran, amefariki. Salamu za rambirambi zinaashiria kwamba alikuwa shujaa kwa baadhi ya watu kadhalika wengine walimchukulia kama muuaji katili. Wanablogu wa Ki-Sri Lanka wanatathmini urithi wa kiongozi huyu wa vita na maana ya kifo chake kwa mustakabali wa Watamil na watu wa Sri Lanka.