Habari kuhusu Wakimbizi

Uanaharakati na Umama Barani Asia

  24 Oktoba 2009

Je, mwanamke anatoa sadaka zipi ili kupigania jambo analiamini? Je, watoto wake wanaathiriwa vipi na mateso yanayoelekezwa kwake? Makala hii inachambua kwa kifupi maisha ya wanawake wanaharakati katika Asia ambao pia ni ma-mama.

Philippines:Mafuriko Mabaya Zaidi Katika Kipindi cha Miaka 40

  30 Septemba 2009

Kimbunga kilichopewa jina la 'Ondoy" kimeikumba Philippines jumamosi iliyopita na kusababisha mafuriko mabaya zaidi katika kipindi cha miaka 40 ambayo yamesababisha vifo vya watu 50 na kusababisha wakazi 280, 000 kupoteza makazi. Tovuti za kijamii zilipashana habari za kimbunga hicho na jinsi ya kuwasaidia walioathirika.

Sri Lanka: Wanablogu Watathmini Kifo cha Kiongozi wa LTTE

  19 Mei 2009

Serikali ya Sri Lanka imetangaza kwa kupitia vyombo vya habari vya taifa pamoja na ujumbe wa simu za mkononi mchana leo (Jumatatu, 18 Mei, 2009) kwamba kiongozi wa Kundi linalotaka kujitenga la Wa-Tamil, the Liberation Tigers of Tamil Eelam (LTTE), Vellupillai Prabhakaran, amefariki. Salamu za rambirambi zinaashiria kwamba alikuwa shujaa kwa baadhi ya watu kadhalika wengine walimchukulia kama muuaji katili. Wanablogu wa Ki-Sri Lanka wanatathmini urithi wa kiongozi huyu wa vita na maana ya kifo chake kwa mustakabali wa Watamil na watu wa Sri Lanka.