
Picha iliyowekwa kwenye mtandao wa facebook na Mwandishi wa Habari wa Rais Don Wanyama ikimwonesha Rais wa Uganda Yoweri Museveni akiongea na simu pembeni mwa barabara.
Watumiaji wa mtandao wa Twita walitumiana picha za kuchekeshana baada ya kuonekana kwa picha inayomwonesha Rais wa Uganda Yoweri Museveni akiwa amekaa kwenye kiti chake pembeni mwa barabara akiongea na simu. Msafara wake, ambao ulikuwa ukielekea kwenye shughuli ya kikazi, ulisimama kwa takribani dakika 30 kumsubiri apige simu.
Mwandishi wa Habari wa Rais Don Wanyama aliweka picha hiyo kwenye ukurasa wake wa facebook ikiwa na maelezo yafuatayo:
Njiani kutoka Wilaya ya Isingiro jana ambapo alishiriki maadhimisho ya Siku ya Idadi ya Watu Duniani, Rais Museveni alisimama kwenye kijiji cha Kyeirumba ili aweze kupiga simu. Wakazi wa eneo hilo waliokuwa wakijiuliza nini kinaendelea walikusanyika kumwona Rais, ambaye baada ya dakika 30 za kuzungumza na simu, alijichanganya nao kwa muda mfupi. Waliishukuru serikali kwa kuweka lami barabara iyo inayounganisha Uganda na Tanzania kupitia Isingiro.
Baadhi ya watu walikuwa na wasiwasi kuwa huenda picha hiyo ilikuwa sehemu ya mpango wa kuwafanya watu wasijadili habari za kuachiliwa huru kwa mwanasiasa wa upinzani Kizza Besigye, aliyekuwa kizuizini kwa muda wa miezi miwili akikabiliwa na mashtaka ya uhaini.
But the #M7Challenge was too strategic to overshadow the release of Besigye dominating the internet 😊😊
— Daron (@bartlettdaron) July 13, 2016
Picha na mjadala huu kumhusu Museveni ni mkakati wa kufunika tukio la kuachiliwa huru kwa Besigye lisijadiliwe kwa uzito mtandaoni
ALama ishara ya#ShindanolaM7 imetumiwa kuonesha picha za wa-Ganda na watu wengine duniani kote wakizungumza na simu zao pembeni mwa barabara. Rais Museveni anajulikana kwa jina la utani la M7 kwa sababu ya matamshi ya jina lake. Watumiaji wengine wa mtandao wa Twita wamekuwa wakiweka picha zilizohaririwa kumdhihaki rais huyo.
Haifahamiki Museveni alikuwa akizungumza na nani hasa wala kiini cha mazungumzo hayo.
Mtumiaji wa Mtandao wa twita aliamini kwamba Museveni alikuwa akizungumza na viongozi nchini Sudani Kusini, ambako mapigano yamelipuka:
#M7Challenge : It is possible M7 was having a “Let my people go” discussion with the leaders of #SouthSudan.
— Frank Hook (@FrancisHookDF) July 13, 2016
Inawezekana M7 alikuwa na majadiliano ya “waachieni watu wangu waende zao” na viongozi wa Sudani Kusini
Museveni ameamuru jeshi la Uganda kuwaondoa wa-Ganda wanaoishi Sudani Kusini kufuatia mapigano yanayoendelea kwenye mji mkuu wa nchi hiyo, Juba.
Rosebell Kagumire aliwaonya washiriki wa #ShindanolaM7 kutokujaribu kufanya kitu kama hiki:
Don't try this at home. First contact the #M7Challenge wealth creation team 😝😝 pic.twitter.com/Jzrh3H2d1q
— Rosebell Kagumire (@RosebellK) July 12, 2016
Usijaribu hili nyumbani. Wasiliana kwanza na timu ya ubunifu ya #ShindanolaM7
Fredrick Tumusiime aliweka linalodaiwa kuwa tangazo la kituo kimoja cha televisheni nchini Uganda:
Before @ntvuganda takes down the tweet☺ #M7Challenge pic.twitter.com/wwJG8xzcmD
— Fredrick Tumusiime (@tufre80) July 12, 2016
Kabla @ntvunga hayaifuta twiti yake
Watumiaji wengine wa Twita walitoa nje viti vyao vya ofisini ili kupiga simu:
@nbstv #M7Challenge pic.twitter.com/coKcBOWkpi
— Nimu Githahu (@wairimugithahu) July 13, 2016
Mathias Wandera alijaribu kumwonesha Museveni akipiga simu akiwa mwezini:
Hehehh 😂😂. Sevo going places. Now he's on the moon. Hater gonna say its photoshop. #M7Challenge pic.twitter.com/L5NT5r6gdI
— Mathias Wandera (@Nva_Kampala_23) July 13, 2016
Sevo uko juu. Wasiompenda watasema picha hii ya kutengeneza
Shidnano hilo, kama anavyolitazama AutoblogKE, ni kuwakumbusha madereva:
haha guys who can pull the best #M7Challenge ?? i think it would be a good way to say STOP TEXTING/CALLING WHILE DRIVING
— AutoblogKE (@AutoblogKE) July 13, 2016
Ha ha jamani nani anaweza kushinda shindano hili? Nadhani ni namna nzuri a kusema TUSIENDESHE HUKU TUKIANDIKA SMS/KUPIGA SIMU
Omara Ronnie alituma picha yake ya #ShindanolaM7 akiwa kwenye kijinjia kidogo kuonesha heshima aliyonao kwa watumiaji wote wa barabara:
All are roads… showing respect to all road users. My #M7Challenge @UNRA_UG @roadsafety @KagutaMuseveni pic.twitter.com/3gd16lnFjv
— Omara Ronnie (@Ronnie_Ug) July 13, 2016
Zote ni barabara…heshima kwa watumiaji wote wa barabara
iAfrikan alionesha picha ya timu ya taifa ya Ureno ikishangilia ushindi wa kombe la Ulaya wakati Museveni akiendelea kuongea na simu:
“Haters are going to say it's photoshop”
📷 @mwanjalouis #M7Challenge pic.twitter.com/m1CPiPJF6u
— iAfrikan (@iafrikan) July 12, 2016
“Wasio mpenda rais watasema picha hii ni ya kutenegeneza”
Mathias Wandera aliweka picha ya Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe akiwa amepiga magoti mbele ya Museveni:
Museveni memes continue for another day?? Heehe 😂😂. Cool lets do this. #M7Challenge pic.twitter.com/ma6oHhKxp9
— Mathias Wandera (@Nva_Kampala_23) July 13, 2016
Picha za Museveni bado zinazunguka? Hehehe. Ngoja nijaribu hii.
Ory Okolloh Mwangi aliweka picha hii ikiwa na muhusika wa filamu ya Game of Thrones
Runner up. 😂 #M7Challenge pic.twitter.com/52yyzDsCoB
— Ory Okolloh Mwangi (@kenyanpundit) July 12, 2016
Picha ya Mshindi wa Pili
Watoto hawakuachwa nyuma:
#M7Challenge has taken up another twist… pic.twitter.com/sZ8naXDKqd
— Ayella (@AyellaBryanLama) July 13, 2016
Shindano limechukua sura mpya
Wakati huo huo, Michael Kwambo anasubiri zamu yake ya kushiriki shindano hilo:
Guys…please let me know when its my turn for the #M7Challenge ..let me patiently wait… pic.twitter.com/NbeoXDCH1E
— Michael Kwambo ™ (@michaelkwambo) July 13, 2016
Jamani…tafadhali nijulisheni lini zamu yangu itafika nishiriki shindano…naomba nilisubiri kwa hamu