Kwa nini Kila Mtu Nchini Madagaska Anafanyia Mzaha Mananasi

I am #Pineapple via Mirana (with permission)

Nanasi la Je suis, au mimi ni nanasi. Picha ya Mirana (imetumiwa kwa ruhusa)

Linapokuja suala la mzaha mtandaoni, basi nanasi limekuwa kama chungwa jipya, angalau kwa nchi ya Madagaska.

Mitandao ya kijamii nchini Madagaska imejawa na mzaha wenye kibwagizo cha nanasi kwa siku kadhaa sasa. Kwa nini tunda hili lenye miiba miiba limekuwa na umaarufu wa haraka hivyo? Hii ni sehemu tu ya hali halisi katika jamii hiyo iliyo ndani ya kisiwa hicho Chekundu.

Madagaska inaonekana kuwa kati ya nchi masikini zaidi duniani baada ya Benki ya Dunia kuchapisha takwimu zake na (kuripotiwa na vyombo vya habari kama vile Radio France Internationale). Ukosoaji juu ya hali ya uchumi wa nchi haukumpendeza sana Rais wa Madagaska. Aliwaomba wachambuzi, vyombo vya habari na wananchi “ kutoa ushahidi unaoonesha kuwa nchi hiyo inaendelea kuwa masikini zaidi.”

Watumiaji wa mitandao ya kijamii wa ki-Malagasiharaka walilitazama suala hilo kwa namna rahisi:

Je takwimu hizi si ushahidi unaojitosheleza Mheshimiwa Rais? #Madagascar #WASH

Koolsaina, Blogu ya kijamii ya Malagasi ilibandika picha ifuatayokatika tovuti yake:

Wananchi wa Malagasi wakipekua vitu katika marundo ya takataka katika jalala mjini Antananarivo via koolsaina

Wananchi wa Malagasi wakipekua vitu katika marundo ya takataka katika jalala huko mjini Antananarivo. Picha ya Koolsaina

Kufuatia majibizano makali yaliyotokea baina ya Rais na mitandao ya kijamii ya Malagasi, tovuti nyingine ya kijamii, Tananews, ilibandika picha ya mke wa Rais Voahangy Rajaonarimampianina akiwa amevaa nguo ya kijani ikiwa na urembo wenye picha ya nanasi kwa mbele:

Rais na mkewe wakiwa katika sherehe za siku ya Uhuru via Tananews

Rais wa Malagasi akiwa na mkewe katika sherehe za siku ya Uhuru. Picha na Tananews

Tananews waliweka ukurasa mwingine ukiwa na maneno ya mzaha yaliyosema, “Hakika, sio kila mtu ni maskini hapa Madagaska.” Katika ukurasa huo walionesha gauni alilovaa mke wa Rais lililobuniwa na kampuni kubwa ya ubunifu wa mavazi ya Dolce & Gabana na linauzwa dola $7,745 katika tovuti ya idara ya mauzo Nieman Marcus (hakuna uhakika kama hiyo ndio bei halisi ya gauni hilo alilovaa mke wa Rais).

Kulitokea ghadhabu ya ghafla katika mitandao wa intaneti nchini humo. Mafuriko ya utani huo wenye alama ishara ya #mananasi yameendelea kwa siku kadhaa ndani ya tovuti mbalimbali na mitandao ya kijamii ya Malagasi. Hii ni baadhi tu ya mizaha iliyotumiwa na kuenezwa kwa wingi:

Kibonzo cha Marc Zuckerberg akishangaa kuhusu mananasi huko Madagascar (with permission)

Kibonzo cha Marc Zuckerberg mwanzilishi wa Facebook akishangaaa kuhusu mananasi huko Madagaska. Kibonzo kinasomeka hivi, Je unajua jinsi ya kuvaa nanasi kama wafanyavyo huko Antananarivo ? (Cheza na maneno kwa kutumia nyimbo za asili)” Imetumika kwa ruhusa.

 

Ombaomba: "Tafadhali, je naweza kupata dola 7,000?quot; Mke wa Rais: " Sina nanasi kwa ajili yako" via POV FB page

Ombaomba: “Tafadhali, je naweza kupata dola 7,000?” Mke wa Rais: “Sina nanasi kwa ajili yako.” Picha imechukuliwa kwenye ukurasa wa Facebook wa POV

" Mkato mpya wa nywele wa nanasi kwa sababu nataka kuwa maarufu pia" via Rivo Francis on Facebook

“Mtindo mpya wa kunyoa nanasi kwa sababu nataka kuwa maarufu pia.” Picha ya Rivo Francis kwenye mtandao wa Facebook

"Je ulifahamu kuwa bradi ya Dolce & Ananas ndio chanzo cha ghadhabu na hasira hapa Madagascar ?" via Aina Rakotoson onn FB

“Je ulifahamu kuwa brandi ya Dolce & Ananas ndio chanzo cha ghasia na hasira hapa Madagaska?” “Anana” ikimaanisha nanasi kwa Kifaransa. Picha yaAina Rakotoson kwenye Facebook

Kwa bahati mbaya, mizaha yote iliyohusu nanasi ilikuja baada kutokea tukio la kutisha katika sherehe za siku ya Uhuru wa nchi hiyo; ambapo, bomu la kurushwa kwa mkono lililipuka wakati wananchi wakiangalia gwaride la kijeshi katika uwanja wa Taifa,na kuua watu watatu na wengine 91 walijeruhiwa. Hii ni video ya tukio hilo

Majadiliano yote ndani ya “Pineapple-Gate” yamekuja katika kipindi muhimu ambapo muswada wa sheria ya uhuru wa kujieleza na maadili mtandaoni  unaandaliwa na mamlaka za Malagasi. Wakizungumzia hilo vyanzo vya ndani vinatonya na kuzungumzia jinsi muswada huu utakavyobana uhuru wa kujieleza mtandaoni na utakuwa na faini kubwa kwa makala au taarifa zozote zitakazoonekana kuwa ni za uongo. Muswada huo utakabidhiwa bungeni wiki chache zijazo kwa ajili ya kupitishwa.

Mhariri wa Global Voices kwa ki-Malagasi Andriamifidisoa Zo kwa jina la utani Jentilisa amechangia habari hii kwa viungo na barua pepe kwa wanablogu waliotajwa kwenye makala haya.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.