Viongozi wa Lumad kutoka kwenye jimbo la Surigao walitaarifu kuwa vikundi vya wanamgambo vilivamia shule zao pamoja na wanajamii, hali iliyolazimu zaidi ya watu 2,000 kuyakimbia makazi yao maeneo ya milimani na kutafuta hifadhi katika maeneo ya jiji. Wengi wao walikuwa watu wa jamii ya Lumad ambao walipinga vikali uvamizi wa makampuni ya uchimbaji madini.
Tume ya Taifa ya Utamaduni na Sanaa (NCCA), moja ya taasisi za serikali, ilielezea kuwa, ukatili dhidi ya Lumad kuwa ni shambulio dhidi ya utamaduni wa Kifilipino:
Tume ya Taifa ya Utamaduni na Sanaa (NCCA) inawatambua raia hawa wazawapamoja na viongozi wao kama kiini na tegemeo la urithi wa kiutamaduni wa nchi ya Ufilipino. Uvamizi huu ni kikwazo dhidi ya utamaduni wetu wa kipekee wa kisanaa. Ukatili wao ni ukatili dhidi ya utu wa watu wetu. Kama watoa elimu wa kipindi kirefu, maarifa na utendaji, kuwajeruhi ni kuharibu msingi wa utamaduni ambao ndio tegemeo la maendeleo endelevu ya nchi yetu.
Kwa siku kadhaa za mwezi Septemba, kiungo habari cha Twitter#StopLumadKillings kilipata umaarufu miongoni mwa raia wa mtandaoni wa nchini Ufilipino pale walipotumia mitandao ya kijamii kama namna ya kuwaunga mkono watu wa jamii ya Lumad waliofukuzwa kwenye makazi yao. Zifuatazo ni baadhi ya picha na jumbe zikionesha kuiunga mkono jamii ya Lumad:
Wanafunzi wa St. Scho-Manila watoa sauti za mfululizo kama namna ya kuunga mkono kampeni ya #StopLumadKillings. | Picha kutoka Edd Gumban pic.twitter.com/CXimqdTcv0
— The Philippine Star (@PhilippineStar) September 15, 2015
Kmpeni ya #StopLumadKillings imeungwa mkono PI na nchi nyingine. Zifuatazo ni picha zinazoonesha mshikamano wa kimataifa uungaji mkono jamii ya Lamad:
Muwakilishi maalum wa umoja wa Maifa wa kuratibu haki za raia wazawa, Victoria Tauli-Corpuz, na mtetezi wa haki za binadamu, Michel Forst walilitaka jeshi kuacha kuzishikilia baadhi ya shule za kiutamaduni:
Hali ya majeshi kushikilia taasisi za kiraia pamoja na kuwaua raia, hususani maeneo kama shule ambazo zilipaswa kuwa sehemu salama kwa ajili ya watoto wa maeneo haya yaliyo na machafuko, ni mambo yasiyokubalika, wala kuvumilika na ni kinyume kabisa na haki za kimataifa za binadamu na pia ni kinyume na viwango vya kimataifa vya utoaji huduma za kijamii
Hata hivyo, jeshi limekanusha kuwa liliratibu makundi mithili ya jeshi kwa ajili ya kuzidhalilisha jamii za watu wa Lumad. Jeshi lilisisitiza kuwa, vita vya kimakabila ndivyo vilivyokuwa chanzo cha machafuko katika maeneo ya Lumad. Lakini, Gavana wa jimbo alitupilia mbali madai haya na kulitupia jeshi lawama kwa kuasisi na kutoa silaha kwa makundi haya mithili ya jeshi. Seneta wa Ufilipino ameahidi kulifanyia uchunguzi suala hili.