Mwanablogu anayeheshimika nchini Misri Alaa Abdel-Fattah amechiwa kwa dhamana akisubiri mashitaka leo -baada ya kukaa gerezani kwa siku 115 akidaiwa kuvunja sheria mpya ya kuzuia maandamano.
Kwa muda wote huu, Abdel Fattah amekuwa gerezani bila kesi yake kusikilizwa.
Video hii, iliyowekwa na Mahmoud Salmani inamwonyesha Abdel Fattah akikaribishw ana familia na marafiki zake baada ya kuondoka kwenye kituo cha polisi:
Na Galal Amr anaweka picha hii inayomwonyesha Abdel Fattah akimkumbatia mke wake Manal Hassan:
Alaa Abdel Fattah (@alaa) released. #Egypt pic.twitter.com/gVERaGb9x9
— Galal (@GalalAmrG) March 23, 2014
class=”twitter-tweet” lang=”en”>
Alaa Abdel Fattah (@alaa) ameachiliwa.
Kwenye twiti yake ya kwanza baada ya kuachiwa, Abdel Fattah anajiapiza “kuendelea”[ar]:
احنا اللي دهنا الهوا دوكو. اتنفخنا بعدها صحيح بس عادي مكملين :-)
— Alaa Abd El Fattah (@alaa) March 23, 2014
“tutaendelea..”
Nadine Marroushi anaitafsiri twiti hiyo:
@Sarahcarr @Fouda_ @_NSalem_ so better translation "we painted the air with doko. true we got fucked afterwards, but we'll continue" ?
— Nadine Marroushi (@nadinemarroushi) March 23, 2014
@_NSalem_ kwa hiyo tafsiri nzuri zaidi; tulipiga rangi hewa kwa kutumia doko. Ni kweli tulifanywa wajinga baadae, lakini tutaendelea.
Doko ni rangi ya kupulizilia kwa lafudhi ya Kimisri.
Zaidi ya Abdel Fattah, Ahmed Abdel Rahman pia aliachiliwa leo. Abdel Rahman, aliyekuwa mpita njia tu wakati wa maandamano, alikamatwa pamoja na Abdel Fattah, alipokuwa akiwasaidia wasichana waliokuwa wanadhalilishwa na polisi.
Kwenye mtandao wa twita, vifijo vilitamalaki.
Ahdaf Souief, shangazi wa Abdel Fattah, anasema kwa furaha:
Twitter is bursting with joy at @alaa's release. My laptop needs a break.
— Ahdaf Soueif (@asoueif) March 23, 2014
Mtandao wa twita unalipuka kwa furaha kufuatia kuachiliwa kwa Alaa. Kompyuta yangu ndogo inahitaji mapumziko
Mona Seif, dada wa Abdel Fattah, alifurahia kuachiliwa kwa kaka yake akisema:
علاء و احمد على الاسفلت … اعظم جملة في الكون :)
— Mona Seif (@Monasosh) March 23, 2014
Alaa na Ahmed wamerudi mtaani…Hii ni sentensi nzito kuliko zote duniani
Pamoja na hati ya kuachiwa kwake, familia ya Abdel Fattah ilisubirishwa kwa masaa nje ya kituo cha polisi ili kumchukua. Seif anaelezea tabu waliyokumbana nayo:
احنا مستنيين لسة عند المديرية و مش فاهمين سبب التاخير و في صحفيين بيتصلوا بيقولوا مصادرهم بتقول هيخرجوا بكرة! احنا خلصنا كل الاجراءات!!!
— Mona Seif (@Monasosh) March 23, 2014
Tumekuwa tukisubiri nje ya makao makuu ya polisi na hatuelewi sababu ya kuchelewa huku. Baadhi ya waandishi wanatupigia simu kutuambia kuwa vyanzo vyao vya habari vinasema ataachiliwa kesho
Na anaongeza:
الكفالات ادفعت، خلصنا الاجراءات في النيابة و القسم و احمد عبد الرحمن خرج في بوكس من القسم من كتير!! ليه التأخير و ليه التعنت في كل خطوة
— Mona Seif (@Monasosh) March 23, 2014
Dhamana imelipwa na tumemaliza urasimu wote na Mwendesha Mashitaka wa Serikali na kituo cha pilisi na Ahmed Abdelrahman ameshuka kwenye gari la polisi na amekuwa kwenye kituo cha polisi kwa muda mrefu. Kwa nini kuna ucheleweshaji na kwa nini kuna vikwazo vingi kwa kila hatua?
The case has been adjourned to April 6.
1 maoni