Habari kuhusu Nchi za Caribiani

Wafalme Watatu Watembelea New York

  14 Januari 2013

Wafalme watatu walikuja na kuondoka, lakini siyo kabla ya kupita katika jiji la New York ili kusherehekea na mamia ya watoto waliojitokeza kwa ajili ya paredi. Shamra shamra hizi za Noeli, kwa karne nyingi, zimekuwa ni sehemu ya utamaduni wa watu wa Amerika wenye asili ya Karibeani na Walatini..The Three Kings came and went, but not before passing through New York City to celebrate with hundreds of children that came out for the parade. This Christmas celebration has been a part of the Caribbean and Latin American cultural traditions for numerous centuries.

Habari za Upotoshaji Kuhusu Afrika Katika Vyombo vya Habari vya Kimataifa

 Kampeni ya kumkamata #Kony2012 ilibeba mambo yaliyorahisishwa mno kuhusu Afrika. Vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe, hata hivyo, kwa sasa havina kinga dhidi ya ukosoaji wa aina hii. Hapa ni muhtasari wa watu maarufu, makosa na kutokuwepo umakini katika habari zinazopewa nafasi katika vyombo vya habari vya dunia kuhusu Afrika na katika vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe

Trinidad na Tobago: Ufisadi na Utawala wa Sheria

  9 Oktoba 2012

Hivi karibuni, masuala ya utawala wa sheria yamekuwa yamekuwa yakitawala serikali iliyoko madarakani. Kwa kuwa na kipengere cha 34 ambacho hakifahamiki sana miongoni mwa wananchi, hali ya mambo imebadilika na kuwa utawala wa kiimla, na […] tunaweza kuona ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka yamebadilisha kabisa tabia za wale tuliowaona...

Paralympiki 2012: Mwanzo mzuri, Habari za Kukumbukwa

  16 Septemba 2012

Martine Wright, aliyenusurika mlipuko wa mabomu uliotokea London, Rim Ju Song, mshiriki wa kwanza kutokea Korea Kaskazini ambaye, miezi michache iliyipita, hakuweza kuogolea; na Hassiem Achmat, ambaye alinusurika kuuawa na papa aliyemshambulia akiwa baharini. Baadhi tu ya washiriki wakuu wa mashindano ya Paralympiki. Martine Wright, aliyenusurika mlipuko wa mabomu uliotokea London, Rim Ju Song, mshiriki wa kwanza kutokea Korea Kaskazini ambaye, miezi michache iliyipita, hakuweza kuogolea; na Hassiem Achmat, ambaye alinusurika kuuawa na papa aliyemshambulia akiwa baharini. Baadhi tu ya washiriki wakuu wa mashindano ya Paralympiki.

Cuba: Maandamano yafanyika Mara Mbili, Wengi Wakamatwa

  7 Julai 2012

Kikundi cha wanawake kijiitacho ‘wanawake wavaliao mavazi meupe’ (Ladies in White) kwa mara nyingine wametawala fikra za wanablogu wa Cuba waishio nje ya nchi. Maandamano ya amani ya kikundi hicho ambacho ni moja wapo ya vyombo vya upinzani vinavyoheshimika zaidi katika visiwa hivyo –pamoja na kukamatwa kwao mara kwa mara na vyombo vya dola –yanaendelea kuvuta hisia za watu. Mapambano ya hivi karibuni yalitokea mwishoni mwa juma lililopita wakati wanachama wa kikundi hicho walipojaribu kufanya maandamano mara mbili mjini Havana.

Global Voices: Changia Leo

2011 umekuwa mwaka usio wa kawaida katika maudhui ya mtandaoni. Global Voices imekuwepo pale wakati mapinduzi yalipotokea, wakati tawala za kidikteta zikianguka, na matokeo ya matumizi ya mtandao yaliposambaa katika miji na mitaa ya wachangiaji wetu wanaoripoti kutoka duniani kote.

Haiti: Kuokoa Maisha

  20 Novemba 2010

“Idadi ya wagonjwa waliotibiwa katika siku 10 zilizopita ni 227″: matumaini ya kweli kwa haiti wanaeleza uzoefu wao wakati wanasaidia kupambana na ugonjwa wa kipindupindu.

Haiti: Video Inayookoa Maisha

  9 Novemba 2010

Mganga nayeishi jijini Fransisco ambaye pia ni mwanablogu Dkt. Jan Gurley amezuru Haiti mara mbili tangu lilipotokea tememeko la ardhi la Januari 12 ili kuwahudumia watu kwa kujitolea. Ziara yake ya pili ilikutana na tukio la maambukizi ya kipindupindu ambalo limetwaa maelfu ya maisha na kusababisha maelfu wengine kulazwa hospitali...