Habari kuhusu Nchi za Caribiani kutoka Februari, 2009
Martinique: Uhuru na “Ubeberu” wa Kifaransa
Wakati harakati za wafanyakazi zinaendelea huko Martinique na Guadeloupe, wanablogu wa Martinique wanapima uhuru wa Idara za Ng'ambo utamaanisha nini. Le blog de [moi] anaona dhana ya kuwa Martinique haiwezi kujitegemea ni dhana inayotusi na ya kibeberu. Wasomaji wake wanadhani kuwa ukweli wa kisiwa chochote kidogo ni kuwa kila siku kitakuwa katika kivuli cha wengine.
Guadeloupe: Hali Tete Yazua Ghasia
Baada ya wiki za maandamano ya amani katika Idara za Ng'ambo za Ufaransa za Guadeloupe na Martinique, mambo yaligeuka na kuwa ghasia siku ya jumatatu, polisi na waandamanaji walipambana katika jiji kubwa la Guadeloupe, Pointe-a-Pitre. Wafanyakazi wanapinga ukosefu wa ajira unaoongezeka pamoja na kupanda kwa bei za bidhaa muhimu, ambazo nyingi zake huagizwa kutoka Ufaransa.
Jamaika: Miziki Yenye Maneno Machafu Yazuiwa
Utata wa muda mrefu juu ya usahihi wa kurushwa hewani kwa miziki fulani umezuka tena nchini Jamaika. Wanablogu wa Jamaika wanapaza sauti zao.
Haiti: Fanmi Lavalas na Uchaguzi Ujao
Mwishoni mwa juma lililopita, ulimwengu wa wanablogu wa Kihaiti ulijaa habari za kutengwa kwa vyama vya siasa na Tume ya Muda ya Uchaguzi kwenye uchaguzi wa maseneta utakaofanyika mwezi Aprili 2009 , na siku ya tarehe 6 Januari, tume hiyo CEP ilichapisha orodha ya wagombea ubunge watakaokwaana kwenye uchaguzi ujao wa bunge nchini Haiti. Wanablogu wanaandika mawazo yao kuhusu wagombea walioachwa.
Karibeani Ya Kifaransa: Tamasha la Kanivali 2009 Lazinduliwa
Kanavali ni utamaduni, sehemu ya uhai wa kila Muhindi wa Magharibi bila kuwaacha wale wa Karibeani ya Kifaransa. Ufuatao ni muhtasari wa blogu kutoka Martiniki, Guyana ya Kifaransa, Haiti na Guadalupe, ambao unaelezea mambo yanavyokuwa kwenye Kanivali.