Habari kuhusu Michezo
Levant: Wanablogu wa Mashariki ya Kati Wanajipasha Moto kwa Ajili ya Kombe la Dunia 2010
Kombe la Dunia litaanza katika kama wiki tatu hivi na wanablogu katika mashariki ya kati tayari wameshaanza kutumia vibodi na kamera zao kujaribu kunasa shauku inayoizingira dunia mara moja kila miaka minne. Anas Qtiesh anatuletea maoni ya wanablogu wa Syria na Lebanoni katika makala hii.
Misri: Sisi Ni Washindi
Timu ya kandanda ya Misri iliifunga Ghana katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, na ikapata ushindi wake kwa mara ya tatu mfululizo. Huu pia ni ushindi wa saba tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo kwenye miaka ya hamsini. Wanablogu wanaungana na wananchi wa nchi hiyo kusherehekea mafanikio hayo.
Togo Yaondolewa Kwenye Mashindano ya Kombe la Afrika baada ya Shambulizi Baya
Timu ya Taifa ya Togo sasa imeondolewa rasmi kutoka kwenye mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kufuatia shambulizi lililoelekezwa kwa msafara wa timu hiyo Ijumaa iliyopita katika eneo la Kabinda lililo nchini Angola na ambalo liko kwenye ukanda wa mapigano baina ya vikosi vya serikali na vile vya waasi wanaotaka kujitenga. Huku kukiwa na shutuma nyingi kutoka kwenye serikali ya Angola na maafisa wanaosimamia soka barani Afrika, wanablogu wa Ki-Togo wanauliza maswali magumu kuhusu msiba huo.
Angola: Kombe La Mataifa ya Afrika Moja Kwa Moja Kwenye Mtandao
Pata habari za Kombe la Mataifa ya Afrika yanayofanyika nchini Angola moja kwa moja: “Kwa wale ambao wangependa kuangalia Kombe la Mataifa ya Afrika 2010 kwenye mtandao, kutakuwa na tovuti za michezo zinazotoa mtiririko wa mapambano ya mpira moja kwa moja mtandaoni, bure.”
Misri na Aljeria: Pambano la Twita
Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini.
Algeria-Misri: Ugomvi Juu ya pambano la Mpira kwenye Mtandao
Hali tete kati ya mashabiki wa mpira wa miguu wa Misri na Algeria inazidi kukua kabla ya pambano litakalofanyika mjini Cairo tarehe 14 Novemba. Mchuano huo utaamua ipi kati ya timu hizo zitafaulu kwenda kwenye Kombe la Dunia la FIFA Afrika ya kusini mwaka ujao. Misri inahitaji japo ushindi wa magoli mawili ili kulazimisha mchezo wa kukata shauri katika uwanja wa nchi nyingine ambapo Algeria, ambayo imeshindwa kufaulu kwenda kombe la dunia tangu 1986, itapambana ili kutunza nafasi yake ya sasa ya kuongoza katika kundi la wanaogombania nafasi ya kufaulu. Wakati wa kuelekea pambano la Jumamosi, mashabiki washindani wamekuwa wakijiandaa nje ya mtandao wa intaneti, kadhalika katika malumbano makali ya mtandaoni, ambayo yamekua na kugeuka “vita-vya-mikwara-kwenye-mtandao”
Afrika Kusini: Kuvuvuzela au Kutovuvuzela?
Mjadala kuhusu kifaa maarufu kinachoitwa vuvuzela kinachopigwa na mashabiki wa mpira wa miguu Afrika Kusini umetawala katika blogu mbalimbali duniani tangu kuanza kwa Kombe la Mabara la mwaka huu nchini Afrika Kusini, lililohitimika wiki iliyopita. Waandishi wa habari, watazamaji wa televisheni, makocha na baadhi ya wachezaji wa kigeni walitoa wito wa kusitisha matumizi ya kifaa hiki katika Kombe la Dunia la 2010 nchini Afrika Kusini. Mabishano haya yana sauti kubwa kama chombo chenyewe.
Karibeani: Radi ya Bolt Yaipiga Beijing
“Radi ya Bolt” – Picha na hybridvigour. Tembelea mtiririko wa picha zake. Ujumbe huu utakuwa mrefu kama ufupi wa mtoko wa Mjamaika Usain Bolt kuelekea chaki ya ukomo wa mbio za mita 100 na utukufu wa Olimpiki ulivyokuwa mfupi na mtamu – kwa sababu mabloga wa Karibiani bado hawajashuka kutoka...