Habari kuhusu Kihispania kutoka Februari, 2010
Chile: Tetemeko Kubwa la Ardhi lenye Ukubwa wa 8.8 Laikumba Chile
Saa 9:34 usiku kwa saa za Chile, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.8 liliukumba mwambao wa eneo la Maule nchini Chile. Tetemeko hilo liliutetemesha mji mkuu wa Santiago uliopo Kilomita 325 kutoka katika kiini cha tetemeko hilo. Uharibifu mkubwa umeripotiwa nchin nzima, na idadi ya waliofariki inazidi kwenda juu.
Mapinduzi Nchini Niger: Wanablogu Wapumua Pumzi ya Ahueni
Alhamisi Februari 18 mapinduzi ya kijeshi yalifanyika nchini Niger ambayo kwayo Rais Mamadou Tandja alikamatwa baada ya mapambano ya bunduki katika mji mkuu, Niamey. Miezi michache iliyopita Tandja alibadilisha katiba kinyume cha sheria ili ajiruhusu kuongoza kwa muhula wa tatu katika kile ambacho kilionekana kama dhuluma ya halaiki kwenye kura maoni. Wanablogu wanatoa mitazamo yao juu ya maendeleo haya mapya.
Costa Rica: Video za Mtandaoni Zaongeza Vichekesho Katika Uchaguzi wa Rais
Uchaguzi wa Rais wa Costa Rica unafanyika Jumapili hii na kwa kupitia video, wananchi wengi wa Costa Rica wanatoa hisia zao kuhusu wagombea na mustakabali wa nchi yao kupitia vichekesho na utani.