Habari kuhusu Kihispania kutoka Oktoba, 2008
Chile: Mkutano wa McCain na Pinochet Mwaka 1985
Mwaka 1985, Mbunge wa bunge la Marekani aitwaye John Mccain alizuru nchini Chile na kukutana na mtawala wa kiimla Augusto Pinochet, akiwa na viongozi wengine wa serikali. Mkutano huo ambao haujawahi kuripotiwa hapo awali umewekwa wazi na mwandishi wa habari John Dinges, ambaye amechapisha habari hiyo kwenye blogu yake CIPHER [es], kadhalika katika blogu ya Huffington Post, ambako huwa anaandika masuala yanayomhusu John McCain "ambaye amekuwa akishutumu vikali dhana ya kuketi na watawala wa kiimla bila ya masharti yoyote, inaonekana kuwa alifanya jambo hilo hilo analolipinga.
Marekani ya Kusini:Taarifa,Twita kwa Waandishi wa Habari Yapata Umaarufu
"Reporting On" ni zana mpya ya kublogu kwa kifupi na inachukua umaarufu mkubwa katika kundi la wanahabari wa Marekani ya Kusini (Walatino) ambao wanatumia zana hii ili kupashana habari na wengine kuhusu yale wanayoyaandika.