Kilichotokea Mbwa ‘Mjamzito’ Alipozikwa Hai huko Voronezh

Screen capture: Moye! Online / YouTube

Picha Kutoka Video ya You Tube: Moye! Online / YouTube

Wakazi katika jengo la makazi ya kukodisha huko  Voronezh walifanikiwa kumuokoa mbwa aliyekuwepo kwenye hali ngumu ya kushindwa kujinasua.  Mapema wiki hii, wafanyakazi wa ujenzi,iligundulika kuwa walimfukia mbwa ardhini walipokuwa wakifanya maboresho ya lango la kuingilia la jengo la makazi ya kupanga. Wapangaji wanasema kuwa, mnamo tarehe 22, Septemba, walianza kusikia sauti ya mbwa kubweka na kutoa sauti iliyoashiria kuhitaji msaada ambayo haikusikika vizuri kutoka chini ya matofali yaliyokuwa yametandwazwa siku za hivi karibuni.

Kwa siku mbili, mamlaka husika hazikuweza kujitokeza kwa ajili ya kutoa msaada. Hatimaye, siku ya Alhamisi, Septemba 24, wapangaji kadhaa waliamua kuchukua hatua kwa kuyaondoa matofali na kisha kumtoa mbwa huyo na ambaye aligundulika kuwa alikuwa na mimba. Picha za uokozi kwa haraka zilipata umaarufu katika mitandao ya kijamii, ambapo kwa chini ya masaa 48, zilikwisha kutazamwa na watu zaidi ya 77,000.

Jumuia ya wazawa ya kutetea haki za wanyama inayofahamika kama “Right to Life (Haki ya Maisha”)” imechukua jukumu la kumhifadhi mbwa huyo kwa muda, na pia kuanzisha kampeni ya kumpatia mbwa huyo makazi yake  mapya. Kwa bahati mbaya  watoto wa mbwa huyo(aliyepewa jina la Belka, au “Kichakoro/Kuchakoro”) walipoteza maisha kutokana na msongo pamoja na kupoteza maji mengi baada ya kunaswa ardhini. Kwa sasa, mbwa huyo yupo kwenye kliniki kwa ajili ya ungalizi wa karibu, ambapo wataalamu wa mifugo walifanya utabibu wa mionzi na kumhasi.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.