Chemsha Bongo: Je, Uko Kwenye Hatari ya Kugeuka Gaidi?

"I hope you realize that if they deploy the fried mozzarella cheese sticks, I'm switching teams." tweeted by Twitter user @LibyaLiberty

“Ninatumaini unajua kwamba kama wanapanga mishikaki ya siagi za kukaanga, ninabadili washirika.” anatwiti mtumiaji wa mtandao wa twita @LibyaLiberty

Juma hili, The Intercept ilibaini mfumo wa maswali kwamba serikali ya Marekani inawahamasisha watu wa ustawi wa jamii, walimu na polisi kutumia maswali fulani fulani ili kuwabaini magaidi. 

Mfumo huo unatarajiwa “kuwaweka maafisa wa serikali ya Marekani katika hali ya tahadhari kwa watu wenye hatari ya kugeuka kuwa watu wa ghasia, na familia au jamii zilizo kwenye uwezekano wa kukumbatia itikadi za kikaidi.”

Maswali hayo yaliyochambuliwa kwenye karabrasha la ndani ya serikali lenye kurasa 36 lilipatikana kupitia jarida moja la mtandaoni na lilipangiliwa na Kituo cha Taifa cha Kupambana na Ugaidi  ni sehemu ya mkakati mpana wa serikali wa  Kupambana na Itikadi Kali, unatoa mwito kwa jamii na viongozi wa dini wa kila mahali kufanya kazi na mashirika ya kiserikali na kusimamia sheria .

Ikulu ya Marekani hivi sasa ni mwenyeji wa  mkutano wa kimataifa wa siku tatu kuhusu Kupambana na Itikadi kali ukiwa na wawakilishi kutoka kwenye nchi zaidi ya 60. 

Kwenye kipengele kama “Kuonesha Kukata tamaa, Kutokujiamini,” “Kuzungumizia Kujidhuru au Kuwadhuru wengine,” na “Kujitambulisha na Makundi (Rangi, Utaifa, Dini, Kabila),” maswali hayo yanawaomba walimu, ustawi wa jamii na maafisa wa polisi kuwapa alama watu kati za 1 na 5.

Wakati tukizoma karabrasha hilo, hatukujizuia isipokuwa kucheka kwa sauti kwa sababu ya mtindo wa kupunguza mambo unaotumika kwenye utafiti huo. Tuliamua kutengeneza chemsha bongo yetu wenyewe kwa kutumia bashiri nyepesi zilizofanywa na Kituo cha Taifa cha Kupambana na Ugaidi kwenye kutunga maswali yake. 

Shiriki Chemshabongo yetu ya Kukuchekesha.



Chemshabongo hii imeandaliwa na Taisa Sganzerla, Elizabeth Rivera, Amira Alhussaini naSahar Habib Ghazi.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.