Inataarifiwa kuwa watu 500,000 wameshindwa kutoka katika vijiji wanavyoishi huku wakikosa huduma ya umeme, nishati ya gesi pamoja na maji hali iliyotokana na kutanda kwa theluji mwisho wa wiki hii Kaskazini mwa nchi ya Iran katika majimbo ya, Gilan na Mazandaran.
Afisa mmoja alisema kuwa hili ni anguko kubwa la theluji ambalo halikuwahi kutokea kwa miaka 50 iliyopita. Hadi sasa, maelfu ya watu wameshaokolewa na kupelekwa kwenye makazi ya muda au kulazwa hospitalini.
ZA1-1RA alitwiti:
من ازین باباتم خیالم از خونواده جمه که می دونم اندازه چن ماه برنج دارن #برف #شمال :|
— ZA1-1RA (@zara_esm) Tar 3 Februari, 2014
Sina shaka na familia yangu, wana hifadhi ya kutosha ya mchele kwa matumizi ya miezi kadhaa.
Farshad Faryabi alitwiti:
فکر کنم #وزیرخارجه #سوئد برنگرده از ایران چون الان #برف و سرما تو #ایران بیشتر از سوئد شده :)
— Farshid Faryabi (@F_Faryabi) Tar 3 Februari, 2014
Waziri wa mambo ya nje wa Swiden, Carl Blidt, [aliyeko safarini nchini Iran] hataweza kurudi Swiden kutoka na hali tete ya theluji nchini Iran.
Soheila Sadegh alitwiti:
به علت بارش برف در شرق #گيلان، یک مدرسه ابتدایی بدلیل فرسودگی تخریب شد #آموزشپرورش #مدارس #دانشآموز #معلم #مازندران #رشت #گرگان #اردبيل
— soheila sadegh (@Soheila_Sadegh) tar 3Februari, 2014
Theluji nzito yaharibu vibaya shule huko Gilan.
Maysam Bizar alitwiti:
شهروند #مازندرانی: بخاطر #برف 6 عدد آب معدنی کوچک 3 هزار تومانی را خریدیم 12 هزار تومان. خودمون به خودمون رحم نمیکنیم از دشمن انتظار داریم؟
— Maysam Bizar (@M_Bizar) tar 3 Februari, 2014
Gharama ya maji ya chupa yalipanda mara nne zaidi ya bei ya kawaida katika kipindi cha tatizo la theluji. Kama hatuwezi kujihurumia, labda cha kufanya ni kutegemea maadui?
Mozdeh A alitwiti:
هر چی برا بقیه دنیا نعمته واسه ایرانی جماعت نکبته #برف
— mozhdeh A (@MozhdehT) tar 3 Februari, 2014
Kilicho na Baraka kwa wengine, kwetu ni laana.
Saham Borghani mwezi uliopita (tar 10 Januari) aliweka picha ya chain a barafu.
#برف و #چای pic.twitter.com/6phbpubCjJ
— saham Boorghani (@sahamedin) tar 10 Januari, 2014
2 maoni