Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Sheria
Caribbean Yajiunga na Kampeni ya #BringBackOurGirls
Kama watoto wetu wangetoweka tungelipenda dunia yote kusimama na kuja kutusaidia kuwatafuta wao. Sisi … tunauliza kwamba … kwa nini mara nyingi miili ya wanawake huwa uwanja wa vita ambapo vita hupiganiwa. Hili si tatizo ambalo linahusisha mji mdogo nchini Nigeria, ni tatizo la wasichana wote kila mahali. Tillah Willah...
Sio Rahisi Ukiwa Mtu Mweusi Nchini Cuba
Habari mbaya kwa Wa-cuba wenye ngozi nyeusi au yenye mchanganyiko wa weusi na weupe ni kwamba hakuna taasisi huru za kisheria itawalinda kutelekezwa na serikali. Iván anaripoti kuwa watu wasio wazungu bado wanaendelea kubaguliwa nchini Cuba.
Asilimia 20-40% ya Fedha Katika Sekta ya Maji Barani Afrika Hupotelea kwa Utoaji Rushwa
Mustapha Sesay, Balozi wa Uadilifu wa Afrika Magharibi aliandika kuhusu ufisadi katika sekta ya maji kwenye mtandao wa Waandishi wa Habari wa WASH wa Afrika Magharibi : Suala la upatikanaji wa maji safi na kwa bei nafuu ni haki ya kibinadamu lakini hii haijapewa kipaumbele inavyohitajika sana. Utoaji rushwa katika...
Je, Sheria Mpya ya Ubakaji India Inawasaidia Wanawake?
Tumepata sheria ambayo inaelekeza kuadhibu ubakaji, na ambayo imebanua tafsiri ya ubakaji na kujumuisha watu wengi zaidi – wakati tatizo kubwa lilikuwa kwamba watu waliokuwa wanabakwa kwa mujibu wa tafsiri na adhabu za zamani hawakuwa wanatendewa haki katika nchi ambayo kuna ubakaji kw akila dakika saba, lakini hakuna hata tukio...
Trinidad na Tobago: Tume ya Mapinduzi
Je, Trinis inajali ripoti ya dat de iliyotolewa na Tume ya kuchunguza jaribio la mapinduzi ya Abu Bakr mwaka 1990 ambayo ndio kwanza imetoka? Trini inapendekeza kwamba kutolewa kwa matokeo haya kunaweza kuchukuliwa kuwa ni ya kiwango cha chini, na yamekuja kwa kuchelewa.
Msichana Nchini Madagaska Ajiua Baada ya Picha Zake Kusambazwa Facebook
Koolsaina anaandika kwamba msichana mmoja wa ki-Malagasi alijiua [fr] baada ya picha zake kusambazwa kwenye ukurasa wa Facebook unaoonyesha picha za wasichana wa Madagaska bila ruhusa yao. Wito ulitolewa kwa utawala wa Facebook ulitolewa ili kuufunga ukursa huo. Mpaka leo (Machi 16, 2014), Koolsaina anasema ukurasa huo bado unapatikana.
Kuumaliza Umasikini Nchini Malaysia
Kikundi cha Saya Anak Bangsa Malaysia kinashinikiza kupitishwa kwa Sheria ya Ujumuishi wa Kijamii ili kutatua tatizo la umasikini nchini Malaysia: Maelekezo yatokayo juu kuja chini yanaonekana kutokufanya kazi pamoja na madai tofauti ya serikali. Ili misaada ifanye kazi kweli, basi iende kupunguza ‘maumivu binafsi ya mfukoni’ kwa sababu kila...
Matukio ya Ghasia Zinazofanywa na Majeshi ya Urusi nchini Ukraine
Blogu maarufu ya “Tafsiri za Maida ilichapisha bandiko la mtandao wa Facebook la Dmitry Tymchuk, Mkuu wa Kituo cha Ukraine cha Stadi za Siasa za Kijeshi, linaloeleza matukio ya ghasia za kimataifa zinazodaiwa kufanyika na “matendo yasiyo ya kawaida” tangu Februari 2014. Tymchuk anaanza uchambuzi huu kwa kusema: Kwa mfano,...
Hali ya Uhuru wa Dini Nchini Maldivi
Maldivi ni miongoni mwa nchi za kwanza kwenye orodha ya serikali zinazozuia uhuru wa dini. Ni lazima raia Wamaldivi wawe Waislamu, na hawawezi kufuata dini yoyote isipokuwa Uislamu. Wageni wasio Waislamu hawawezi kupiga kura, kuabudu hadharani, kupata uraia, wala kutumikia umma. Kwa maoni ya Mwanahabari Hilath Rasheed, huenda nchi ya...
Misri: Kampeni kwa Ajili ya Haki za Watu Wenye Mahitaji Maalum
Wamisri pembezoni wenye mahitaji maalum wamekuwa wakifanya maandamano kwa haki zao kabla na tangu mapinduzi ya #Jan25. Hata hivyo, malalamiko yao bado hayajatatuliwa. Wakati Kamati ya watu 50 wanapiga kura juu ya rasimu ya hivi karibuni zaidi ya Katiba ya Misri, kampeni ya Zayee Zayak, ambayo hutafsiriwa kuwa “Mimi ni...