Asilimia 20-40% ya Fedha Katika Sekta ya Maji Barani Afrika Hupotelea kwa Utoaji Rushwa

Upatikanaji wa maji ni haki ya binadamu. Chanzo: actionaid.org kwa ruhusa

Mustapha Sesay, Balozi wa Uadilifu wa Afrika Magharibi aliandika kuhusu ufisadi katika sekta ya maji kwenye mtandao wa Waandishi wa Habari wa WASH wa Afrika Magharibi :

Suala la upatikanaji wa maji safi na kwa bei nafuu ni haki ya kibinadamu lakini hii haijapewa kipaumbele inavyohitajika sana. Utoaji rushwa katika sekta ya maji ni jambo la kawaida na inahusisha madaraja yote ya watu kuanzia mtu wa kawaida, wanasiasa, Wakuu wa Taasisi ya Maji na hata mashirika yasiyo ya serikali wanaofanya kazi katika hii sekta. Ripoti juu ya “Utoaji rushwa katika sekta ya maji” kupitia mtandao wa Uadilifu wa maji katika kitabu chenye jina la “Mafunzo ya Mwongozo wa Uadilifu wa maji ” inasema kwamba katika jangwa la Sahara Afrika, asilimia arobaini na nne (44%) ya nchi haina uwezekano wa kufikia lengo la Maendeleo ya Milenia la upatikanaji wa maji ya kunywa, asilimia themanini na tano (85%) hawana uwezekano wa kufikia kipengele cha usafi wa mazingira. Makadirio ya ripoti ya Benki ya Dunia inaonyesha kwamba asilimia (20 – 40%) ya fedha za sekta ya maji zinapotea kupitia mazoea ya udanganyifu.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.