Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Siasa
Jinsi Wanablogu Walifikia Gerezani kwa Kuandika Kuhusu Haki za Binadamu Nchini Ethiopia
Melody Sundberg anachambua uhuru wa kujieleza nchini Ethiopia baada ya wanablogu wa Ethiopia waliokamatwa kukaa siku 100 gerezani: Ethiopia ina idadi ya watu 94,000,000 na ni nchi ya pili yenye wakazi wengi katika bara la Afrika. Hata hivyo, hailingani na mahojiano ya Endalkhachew Chala kupitia Global Voices, kuwa na gazeti...
Habari Mpya za Mgogoro wa Kisiasa Lesotho Kupitia Twita
Mfuatilie @nthakoana (Nthakoana Ngatane) kupata habari mpya zinazohusu mgogoro wa kisiasa nchini Lesotho. Nthakoana Ngatane ni mwandishi, msemaji, mwimbajii, mwigizaji na mwakilishi wa SHirika la Habari la Utangazaji la Afrika Kusini nchini Lesotho. Mnamo tarehe 30 Agosti 2014, Waziri Mkuu wa Lesotho Tom Thabane alidai kulikuwa na jaribio la kumpindua...
Je Kulikuwa na Jaribio la Mapinduzi Nchini Lesotho?
Sikiliza sauti inayoelezea kile hasa kinachoendelea nchini Lesotho kufuatia madai ya mapinduzi ya kijeshi: Waziri mkuu amekimbilia nchini Afrika Kusini na anasema ni mapinduzi ya kijeshi. Jeshi la Lesotho linasema sio mapinduzi. Siasa zinazua utata. African Defence Review inazungumza na KRISTEN VAN SCHIE wa SADC na mwandishi DARREN OLIVIER kuuliza...
Baraza la Mawaziri Nchini Zambia Lichunguze Afya ya Rais
Kwa mtazamo wa tetesi zilizoenea sana kuhusu afya ya rais wa Zambia, Michael Sata, Gershom Ndhlovu ana hoja kwamba katiba inalipa Baraza la Mawaziri mamlaka ya kuchunguza afya yake: Mara ya mwisho rais wa Zambia Michael Sata kuonekana hadharani ilikuwa takribani Juni 20 ambapo alikuwa mwenyeji wa ujumbe wa serikali...
Hotuba ya Ushindi ya Rais Mteule wa Indonesia
Rais mteule wa Indonesia Joko Widodo or Jokowi alitoa hotuba ya ushindi akitambua moyo wa kujitolea ulioonyeshwa na wananchi: Uchaguzi huu wa rais umechochea mtazamo mpya chanya kwetu, na kwa taifa letu kwa ujumla. Uhuru wa watu na uwajibikaji wa kisiasa vinashamiri katika nyoyo za kizazi kipya. Moyo wa kujitolea...
Trinidad & Tobago: Je, Kuishi kwenye Enzi za Kidijitali Kunahatarisha Haki yako ya Faragha??
Blogu ya ICT Pulse inapitia taarifa iliyochapishwa hivi karibuni iliyoandaliwa na Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu juu ya haki ya faragha katika enzi hizi za dijitali.
Matamshi Matano ya Kushangaza Kufuatia Kuanguka kwa Ndege MH17 Nchini Ukraine
Wakati kukiwa na hisia zinazozidi kuongezeka kufuatia kuanguka kwa ndege nchi Ukraine, matamshi kadhaa yaliyotolewa na watu maarufu Moscow na Donetsk yamevuta hisia za watu
Wa-Indonesia Wawasha Mishumaa Elfu Moja Ishara ya Amani kwa Palestina
Raia wa Indonesia walikusanyika katikati ya Jakarta, mji mkuu wa nchi hiyo, kuwasha mishumaa 1,000 kupinga mashambulio ya Israel katika ukanda wa Gaza. Indonesia ni moja ya nchi maarufu zaidi kwa wingi wa waumini wa dini ya Kiislam.
Waandishi wa kimataifa Wakashifu Israeli kwa Kuendelea kwa Ujenzi wa Makazi
Waandishi kumi na sita wa kimataifa ambao walishiriki katika Tamasha la Wapalestina la Fasihi, lililofanyika katika miji kadhaa Palestina kuanzia Mei 31 hadi Juni 5, walitoa taarifa kukashifu Israeli kwa kuendelea kwa ujenzi wa makazi na kupongeza juhudi za kususia kampeni ya Boycott Divest and Sanction (BDS). Taarifa, kupitia mtandao...
Umuhimu wa Haki kwa Wanablogu wa Ethiopia
Justice Matters ni blogu inayoripoti kuhusu kesi ya wanablogu wa Zone9 waliokamatwa na waandishi wa habari nchini Ethiopia kwa ajili ya kutoa maoni yao: Blogu hii ina habari zaidi za hivi karibuni kuhusu jitihada za utetezi, ripoti za vyombo vya habari, na hadhi ya kisheria ya wanablogu wa Zone9 nchini...