Hotuba ya Ushindi ya Rais Mteule wa Indonesia

Rais mteule wa Indonesia Joko Widodo or Jokowi alitoa hotuba ya ushindi akitambua moyo wa kujitolea ulioonyeshwa na wananchi:

Uchaguzi huu wa rais umechochea mtazamo mpya chanya kwetu, na kwa taifa letu kwa ujumla. Uhuru wa watu na uwajibikaji wa kisiasa vinashamiri katika nyoyo za kizazi kipya. Moyo wa kujitolea uliopotea siku nyingi umerejea tena kwa ari mpya.

Na katika kutangaza “kushiriki katika shughuli za kujitolea”, Jokowi aliwaomba watumiaji wa Facebook kupiga kura na kuchagua mawaziri 34 ambao wanadhani anapaswa kuwaingiza katika Baraza la Mawaziri la serikali yake.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.