Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Kiarabu
Wafanyakazi Wavamia Majengo ya Serikali Nchini Mauritania
Siku ya Jumanne asubuhi, Mei 28, 2013, maelfu ya vibarua, wanaolipwa ujira wao kwa kufanya kazi kwa siku, walianzisha maandamano makubwa [ar] huko Zouérat, mji mkuu wa jimbo la Tiris Zemmour kasikazini mwa Mauritania, wakidai mikataba inayoeleweka na haki zao nyinginezo ikiwa ni pamoja na kumalizwa kwa ukiritimba wa wafanyabiashara...
Tunisia: Mgomo Waanza jijini Thala
Kupitia mtandao wa twita, Tounsia Hourra (m-Tunisia huru) anasema [ar] kuna mgomo mkubwa umeanza jijini Thala, kwenye jimbo la Kasserine, leo [Oktoba 8, 2012]. Mgomo huo umekuja kama hatua ya kupinga kukua kwa kasi kwa ukosefu wa ajira na kuzorota kwa maendeleo ya jiji hilo. @tounisiahourra: اضراب عام في تالة...
Misri: Habari Za Maandamano Ya Upinzani Moja Kwa Moja Kwenye Facebook
Habari za maandamano ya upinzani ya Januari 25 ya vuguvugu la la Vijana wa Aprili 6 zinapatikana kwenye ukurasa huu wa Facebook (Ar). Taarifa zimeibuka leo kuwa Facebook ilikuwa imezuiliwa isipatikane nchini Misri.
Syria: Propaganda ya Vyombo vya Habari vya Serikali Kuhusu Maandamano ya Tunisia na Misri
Mwanablogu wa ki-Syria Maurice Aaek amegundua[ar] kwamba vyombo vya habari vinavyoendeshwa na serikali nchini Syria vinachapisha habari za uongo na nusu-kweli kuhusu maandamano ya upinzani nchini Tunisia na Misri. Amegundua kwamba gazeti la Tishreen daily halikuweka sababu ambazo zilimfanya Ben Ali aondoke na kuwaachia watu wajitafsirie wenyewe, na kuwa gazeti...
Syria: Mwanaharakati wa Haki Za Binaadamu Mwenye Umri wa Miaka 80 Akamatwa
Omar Mushawah ameripoti [ar] kukamatwa kwa Haytham al-Maleh, mwanasheria wa Ki-Syria na mtetezi wa haki za binaadamu ambaye pia alitumia muda wa miaka 6 jela kati ya 1980 na 1986 kwa kudai mabadiliko ya kikatiba. Al-Maleh pia ni mwanzilishi mwenza wa Jumuiya ya Haki za Binaadamu ya Syria.