Jamii, ambazo nyingi ni zile za miliamni au majirani zao, zimekuwa zikitegemea miti na mazao mengine ya asili kutoka porini katika kujikinga au kujitibu magonjwa yao. Lakini uharibifu wa mazingira na kushambuliwa vikali na tamaduni kuu za jamii zinazoishi mabondeni hivi sasa kunatishia mila hizo za tiba.