PICHA: Waandamanaji Nchini Taiwani Wageuza Uzio wa Polisi kuwa Mapambo

Muda mfupi baada ya waandamanaji kuvamia bunge la Taiwani wakipinga makubaliano yenye utata kati ya nchi hiyo na China, mji mkuu wa visiwa hivyo Taipei vilifurika waandamanaji kuanzia Aprili 26 mpaka 30, mara hii wakipinga kiwanda cha nne cha uzalishaji wa nguvu za nyuklia  kinachoendelea kujengwa ingawa inahofiwa kuwa kinaweza kusababisha madhara.

Polisi waliwalazimisha waandamanaji kutawanyika na waliweka miiba na uzio kuwazuia kuzudi. Maandishi yenye maneno chevaux de frise yaliwekwa kuzunguka ikulu ya nchi hiyo, Bunge la Yuani na Majengo ya Serikali ya Yuan pamoja na majengo mengine ya kiserikali. 

Wakijibu hatua hiyo, waandamanaji hao walitumia ubunifu. Walipamba uzio uliowekwa na polisi kwa utepe wenye maneno ya kupinga nguvu za nyuklia, wakaweka mabango ya kisiasa, maua na vitu vingine na hivyo kugeuza miiba iliyokuwa imewekwa na polisi kuwa kama maonyesho ya kazi ya sanaa. Watumiaji wengi wa mtandao nchini humo walitumiana picha zenye mapambo hayo, na hapa chini ni baadhi ya picha hizo:

Alama ya tahadhari iliyoning'inia pembeni mwa uzioikisomeka, “Hatari, usikaribie.” Picha imepigwa na mtumiaji wa Facebook aitwaye Chuan Hsiang Chang, aliyeuita uzio huo ‘waya nyamifu’. CC BY-NC 2.0.

Kasri mvuto la uzingizi, ikulu. Picha na mtumiaji wa mtandao wa Instagram anayejiita deception. CC BY-NC 2.0.

Yapake yawe na wekundu kwa mbali. Picha na mtumiaji wa mtandao wa Twita runst01. CC BY-NC 2.0.

Utepe wa njano. Picha na mtumiaji wa mtandao wa Flickrpbear6150. CC BY-NC-SA 2.0.

Kutuma maua kwa upendo. Picha na mtumiaji wa Flickr live365. CC BY-NC-SA 2.0.

Ndani ya chevaux de frise: waathirika wa utawala wa kiimla. Picha na mtumiaji wa mtandao wa Facebook Wei Hung. CC BY-NC 2.0.

Tutashinda. Picha ya mwandishi wa NTU News E-Forum 張慈安 Tzu-An Chang. CC BY-NC 2.0.

Exit mobile version