Mwanablogu wa ki-Syria Maurice Aaek amegundua [1][ar] kwamba vyombo vya habari vinavyoendeshwa na serikali nchini Syria vinachapisha habari za uongo na nusu-kweli kuhusu maandamano ya upinzani nchini Tunisia na Misri. Amegundua kwamba gazeti la Tishreen daily halikuweka sababu ambazo zilimfanya Ben Ali aondoke na kuwaachia watu wajitafsirie wenyewe, na kuwa gazeti la Al-Baath daily lilisema kwamba maandamano ya upinzani nchini Misri yana nia ya kutaka balozi wa Izraeli afukuzwe, na kutoyaweka kabisa madai ya kutaka Mubarak ang'atuke.
Syria: Propaganda ya Vyombo vya Habari vya Serikali Kuhusu Maandamano ya Tunisia na Misri
· Imeandikwa na Anas Qtiesh Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza
Mada za Habari: Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Misri, Syria, Tunisia, Siasa, Uandishi wa Habari za Kiraia, Vyombo na Uandishi wa Habari