Habari kutoka Aprili, 2010
Indonesia: Sony yamkabili Sony
Sony AK wa Indonesia alitishiwa kushitakiwa kwa kukiuka sheria za matumiza ya nembo na shirika la Sony la Japan kama hatafunga tovuti yake binafsi yenye jina www.sony-ak.com. Suala hili lilizua mwitiko mkali katika jamii ya wanamtandao na kuilazimisha kampuni ya Sony kutupilia mbali shauri hilo.
Moroko: Je, Wakristu Wako Hatarini?
Mapema mwezi Machi mwaka huu, watazamaji walishuhudia jumla ya wafanyakazi wa muda mrefu katika kituo cha Kikristo cha kulelea watoto yatima wapatao 20 wakifukuzwa kutoka katika nchi ambayo wanaiona kama nyumbani. Tukio hilo pamoja na mengine kadhaa yaliyofuatia yamezusha mjadala kuhusiana na imani ya Kikristu katika ufalme huo.
Urusi: Habari za Mwanzo za Milipuko ya Mabomu

Utaratibu wa Jumatatu asubuhi mjini Moscow ulivunjwa leo na milipuko ya mabomu mawili mabomu ya kujiua, ambayo yaliua watu wapatao 38 na kujeruhi kwa uchache watu wapatao 70. Alexey Sidorenko anatafsiri baadhi ya taarifa za mwanzo kutoka katika ulimwengu blogu za Urusi.
Muziki Wenye Ujumbe – Video Mpya za Muziki Kutoka Tibet
Mradi wa kutafsiri Blogu uitwao High Peaks Pure Earth hivi karibuni umetupia jicho “muziki wenye ujumbe” kwa kutafsiri mashairi ya nyimbo za Tibet kutoka video za Muziki zilizowekwa kwenye mtandao....
Tunisia: Wanablogu wa Tunisia Wazungumza Kiingereza
Wanablogu wa Tunisia walizoea kuepuka kutumia Kiingereza (lugha ya tatu nchini mwao), na badala yake waliandika kwa Kiarabu (na wakati mwingine kwa lahaja za Tunisia) au Kifaransa. Lina Ben Mhenni anazitupia macho baadhi ya blogu zinazoandikwa kwa lugha ya Kiingereza.
Chile: Mchakato wa Ujenzi Mpya Baada ya Tetemeko la Ardhi
Mwezi mmoja baada ya tetemeko baya kabisa nchini Chile, Rais Sebastián Piñera ametangaza mpango wa ujenzi mpya wa miundombingu ya nchi na majengo, akiwataka raia wa Chile kutoa mapendekezo jinsi gani mchakato huo utekelezwe na kusimamiwa.