Aprili, 2010

Habari kutoka Aprili, 2010

Indonesia: Sony yamkabili Sony

Sony AK wa Indonesia alitishiwa kushitakiwa kwa kukiuka sheria za matumiza ya nembo na shirika la Sony la Japan kama hatafunga tovuti yake binafsi yenye jina www.sony-ak.com. Suala hili lilizua mwitiko mkali katika jamii ya wanamtandao na kuilazimisha kampuni ya Sony kutupilia mbali shauri hilo.

11 Aprili 2010

Moroko: Je, Wakristu Wako Hatarini?

Mapema mwezi Machi mwaka huu, watazamaji walishuhudia jumla ya wafanyakazi wa muda mrefu katika kituo cha Kikristo cha kulelea watoto yatima wapatao 20 wakifukuzwa kutoka katika nchi ambayo wanaiona kama nyumbani. Tukio hilo pamoja na mengine kadhaa yaliyofuatia yamezusha mjadala kuhusiana na imani ya Kikristu katika ufalme huo.

9 Aprili 2010

Tunisia: Wanablogu wa Tunisia Wazungumza Kiingereza

Wanablogu wa Tunisia walizoea kuepuka kutumia Kiingereza (lugha ya tatu nchini mwao), na badala yake waliandika kwa Kiarabu (na wakati mwingine kwa lahaja za Tunisia) au Kifaransa. Lina Ben Mhenni anazitupia macho baadhi ya blogu zinazoandikwa kwa lugha ya Kiingereza.

7 Aprili 2010