· Oktoba, 2008

Habari kuhusu Ulaya Magharibi kutoka Oktoba, 2008

Bahrain: Raha na Karaha za Kusoma Ng'ambo

  26 Oktoba 2008

Ingawa Bahrain ina idadi kadhaa ya vyuo vikuu, vya umma na binafsi, raia wengi wa nchi hiyo hupata fursa ya kwenda ng'ambo kwa masomo ya shahada ya kwanza na hata zile za juu, mara nyingi kwa kutegemea ufadhili. Moja ya matatizo ya kwanza wanayokumbana nayo huko ughaibuni ni kwamba watu wachache tu hufahamu ni wapi Bahrain ilipo. Katika makala hii tunafuatilia uzoefu wa wanablogu watatu ambao ndiyo kwanza wamekwenda ng'ambo kwa masomo: kule Japan, Uingereza na Marekani na mwanablogu wa nne ambaye anasoma India kwa kipindi fulani hivi sasa.

Madagascar: Kuishi ughaibuni hubadili uhusiano

Katika makala iliyochapishwa mwezi Machi, wachumi William Easterly na Yaw Nyarko wanaeleza kwamba katika nchi zilizo chini ya Jangwa la Sahara, kiasi cha fedha kinachotumwa na wahamiaji wanaotoka bara hilo ni wastani wa asilimia 81 ya misaada ya fedha kutoka nchi za kigeni kwa kila nchi. Dhima ya waMadagascar walio...

Macho ya Kimataifa kwenye Uchaguzi wa Marekani

Kadiri uchaguzi wa Marekani unavyokaribia, ndivyo kadiri macho ya kimataifa yanavyozidi kuelekezwa katika sera za nje za taifa hilo na wagombea wake wakuu. Kazimiradi kama vile ile ya Collective Journalism inayofanywa na Current TV (Uandishi wa Habari wa Umma wa Current TV) na Global Voices' Voices Without Votes (Mradi wa Global Voices - Sauti Zisizo na Kura) zimechukua jukumu la kukusanya taarifa na kuzipa mtazamo wa kimataifa katika masuala ya ndani ya sehemu fulani tu ulimwenguni.