Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Julai, 2012
Somalia: Migawanyiko Mikubwa Kuhusu Katiba Mpya
Somalia, ambayo haijawahi kuwa na serikali kuu inayotawala nchi nzima tangu mwaka 1991, inaandika rasimu ya katiba mpya ambayo inatarajiwa kuhitimisha muda wa utawala wa serikali ya mpito iliyopo madarakani na kumchagua rais mpya. Hapa tumekusanya mijadala na mazungumzo ynayoendelea mtandaoni kuhusu rasimu hiyo ya katiba.
Cameroon: Ndoto za Umeme kwa Ajili ya Maendeleo ifikapo 2035
Cameroon inatarajiwa kufikia hadhi ya soko linalokua kwa kasi ifikapo mwaka 2035 kupitia "mafanikio makubwa" ya hatua kwa hatua katika maendeleo ya miundombinu ya usafiri na nishati. Hata hivyo kufikiwa kwa malengo hayo ndani ya muda uliopangwa hakuonekani kuwashawishi wachambuzi wengi wa masuala ya kisiasa, kwa sababu tu changamoto zilziopo ni nyingi.
Angalia Moja kwa Moja Yanayojiri Sasa Hivi Katika Mkutano wa Global Voices
Mkutano wa Global Voices wa 2012 umeshafunguliwa muda mfupi uliopita katika jiji la Nairobi, nchini Kenya. Tungetamani sana kama ungeweza kujumuika nasi mkutanoni, lakini kama hilo haliwezekani, waweza pia ukatutazama moja kwa moja kupitia mtandao wa intaneti na pia tunaweza kujadiliana moja kwa moja.
Sudani: Maandamano Yachochea Kukamatwa kwa Mwanaharakati wa Twita
Maandamano makubwa yaliyofanyika nchini Sudani siku ya Ijumaa yalisababisha kukamatwa kwa wanaharakati wengi wa nchi hiyo, pamoja na watumiaji maarufu wa mtandao wa twita.