Habari kuhusu Mauritania
Mauritania: Wafanyakazi wa Migodini Wapinga ‘Aina Mpya ya Utumwa’
Zaidi ya wafanyakazi 2,300 wako kwenye mgomo nchini Mauritania katika mji wa kaskazini wa Zouerat, jambo ambalo limesababisha kuzorota kwa maeneo mengine kumi ya Kampuni la Taifa la Madini na Viwanda, huku kazi zikiwa kwenye mvurugiko mkubwa. Madai yamejikita katika suala zima la maslahi bora ya wafanyakazi.
Warsha ya Wanablogu wa Uarabuni: Tafakuri ya Twita kwa Siku ya Kwanza
Wakati siku ya kwanza ya Warsha ya Pili ya Mwaka ya Wanablogu wa Uarabuni ikifungwa, tutaangalia tafakuri za washiriki kwa siku nzima, kujua wamejifunza nini na namna wanavyojisikia. Siku ilianza kwa kishindo, wakati waandaaji wa Global Voices Sami ben Gharbia, Amira Al Hussaini, na wafadhili wetu kutoka Mfuko wa Heinrich...
Mauritania: Uchaguzi wenye udanganyifu?
Tarehe 18-07-2009, miezi 11 baada ya mapinduzi ya kijeshi yakiongozwa na Jenerali Mohamed Ould Abdel Aziz, Mauritania imemchagua Jenerali huyu kwa Urais, na kusababisha wapinzani wakuu wa Abdel Aziz kuukataa uchaguzi kwamba ni “kiini macho,” kwa mujibu wa Habari za BBC. Pitio la haraka haraka kwenye blogu za nchi za Saheli linaonyesha kwamba wapinzani wako katika ushirika mzuri.
Arabeyes: Rais wa Mauritania Aliyepinduliwa Katika mapinduzi ya Kijeshi
MAKAMANDA wa jeshi wamemuondoa madarakani Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi, rais wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa jeshi. Makamanda wa jeshi walitangaza...