Habari kuhusu Malawi kutoka Disemba, 2009

Malawi: Wanablogu Wajadili Matetemeko ya Ardhi 30 Katika Wiki 3

  30 Disemba 2009

Katika kile ambacho baadhi ya wataalamu wa miamba wamekieleza kama matukio ya nadra, Wilaya ya Kaskazini ya Karinga nchini Malawi imeshuhudia jumla ya matetemeko ya ardhi 30 katika wiki tatu zilizopita ambayo yamesababisha vifo 5, zaidi ya watu 200 kujeruhiwa na zaidi ya watu 3,000 kupoteza makazi. Wanablogu wamekuwa wepesi kushirikiana maoni.