Habari kuhusu Madagaska

Madagaska Bado Inasubiri Waziri Mkuu, Serikali Mpya

  26 Februari 2014

Mwezi mzima tangu Rais mteule  Hery Rajaonarimampianina achaguliwe kuwa mkuu wa nchi nchini Madagaska, bado hakuna dalili nani atakuwa waziri mkuu na akina nani wataunda serikali. Ma-Laza anahoji kuwa suala kuu si hasa nani atakuwa waziri mkuu bali atakuwa ana ajenda gani akikabidhiwa ofisi [fr]:   Un  technicien hors pair,  rassembleur,...

Wamalagasi Wajadili Kivazi na Maoni ya Mlimbwende wa Kigeni Kuhusu Madagaska

  23 Februari 2014

Picha ya Tangazo la Kivazi cha Kuogolea 2014 iliyopigwa eneo la (kisiwa cha) Nosy Iranja, Madagaska: Nosy Iranja ni kisiwa kinachofahamika kama Turtle kwa sababu viumbe waitwao Hawksbill Turtles walikuja ufukweni kutaga mayai yao. Kisiwa hicho pia kinafahamika kwa mchanga wa pekee unaounganisha visiwa hivyo viwili. Mlimbende mashuhuri wa ki-Rusi...

Shindano la Kuchochea Uanzishwaji wa Biashara Mpaya Nchini Madagaska

  30 Januari 2014

Harinjaka, mwanzilishi wa mradi wa Habaka na mwanablogu anayeishi Madagaska, ameanzisha Shindano la biashara mpya Antananarivo 2014  [fr] lenye lengo la kuchagua na kuunga mkono wazo la biashara nchini Madagaska. Anaamini kwmaba kuna  mustakabali mzuri kwa ujasiriamali na ubunifu [fr] nchini Madagaskari. Hapa unaweza kuona tangazo la tukio hilo[fr] :   

Maandamano ya Kudai Uchaguzi nchini Madagaska Yasababisha Vurugu

  23 Julai 2013

Blogu ya Vola R ya Ma-Laza inaandika kwamba watu 7 walijeruhiwa [fr] kufuatia matumizi ya nguvu yaliyofanywa na polisi dhidi ya waandamanaji waliokuwa wanadai kufanyika kwa uchaguzi mjini Antananarivo, Madagaska. Chama kinachoongoza maandamano kinasema kwamba utawala uliopo hauna dhamira ya kuitisha uchaguzi mwaka huu na kwamba serikali imeng'ang'ania madarakani. Kiongozi wa...

Wagombea wa Urais katika Uchaguzi wa Madagaska

Habari Mpya:  Hapa ni orodha kamili ya wagombea 49 [fr] wanaowania nafasi ya Urais katika uchauzi ujao. Orodha hiyo haina jina la rais wa sasa wa mpito. Siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi ujao ilikuwa tarehe 28 Aprili, na inavyoonekana ni wagombea wachache sana...

Habari za Upotoshaji Kuhusu Afrika Katika Vyombo vya Habari vya Kimataifa

  31 Disemba 2012

 Kampeni ya kumkamata #Kony2012 ilibeba mambo yaliyorahisishwa mno kuhusu Afrika. Vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe, hata hivyo, kwa sasa havina kinga dhidi ya ukosoaji wa aina hii. Hapa ni muhtasari wa watu maarufu, makosa na kutokuwepo umakini katika habari zinazopewa nafasi katika vyombo vya habari vya dunia kuhusu Afrika na katika vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe

Kitabu-pepe Kipya cha GV: Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko

  30 Disemba 2012

"Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko",  kinakupa mtazamano wa kipekee kuhusu watu na habari za eneo la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia posti zetu zilizo bora zilizoandikwa kwa lugha ya Kiingereza kwa mwaka 2012. Hii ni zawadi sahihi kabisa ya kuukaribisha mwaka mpya.

Kupigia Kura Maajabu Saba ya Dunia barani Afrika

  27 Disemba 2012

Shindano la kila mwaka limezinduliwa kwa ajili ya watu kupiga kura kuchagua maajabu saba yaliyo bora zaidi barani Afrika. Na tayari upigaji kura umeshaanza. Baadhi ya maajabu ya asili yaliondolewa katika orodha ya mwisho ya kupigiwa kura na hivyo baadhi ya wanablogu waliongeza mapendekezo yao katika blogu zao. Tazama baadhi ya picha hapa: