Habari kuhusu Madagaska kutoka Februari, 2009

Madagaska: Zaidi ya 25 Wauwawa Katika Maandamano Kuelekea Ikulu

  9 Februari 2009

Watu wapatao 25 walipigwa risasi na kuuwawa leo katika mji mkuu wa Madagaska, Antananarivo, wakati wa maandamano ya kuelekea ikulu ya nchi hiyo yaliyoitishwa na meya wa jiji Andry Rajoelina baada ya kujitangaza kama kiongozi wa serikali mpya ya mpito katika mkutano wa hadhara wa kisiasa. Katika majuma yaliyopita, ugombeaji wa nguvu za kisiasa kati ya Meya na Rais Marc Ravolamanana kumesababisha ghasia na uporaji.