Habari kuhusu Guinea
Watu Sitini Wauawa Kwenye Mapigano Mjini Nzérékoré, Guinea
Tovuti ya Guinee News inaripoti idadi ya vifo kufikia 60 kutokana na mauaji ya Nzérékoré, Guinea [fr] : Les cinquante deux corps qui étaient non identifiables ont été enterrés dans une fosse commune hier. Les autres corps reconnaissables ont été remis à leurs familles. miili 52 ambayo haikutambulika ilizikwa kwenye kaburi la...
Blogu 10 Bora za Mapishi ya ki-Afrika
MyWeku anatengeneza orodha ya Blogu 10 bora za Mapishiya ki- Afrika kwa mwaka 2013: “Inaonekana kuna blogu milioni moja zinazozungumzia mapishi, lakini ni chache sana zinazoonyesha vyakula vya Kiafrika. Pamoja na hayo imekuwa kazi ngumu kuchagua 10 kati ya nyingi nzuri kwa mwaka huu 2013.”
Mapinduzi Nchini Niger: Wanablogu Wapumua Pumzi ya Ahueni
Alhamisi Februari 18 mapinduzi ya kijeshi yalifanyika nchini Niger ambayo kwayo Rais Mamadou Tandja alikamatwa baada ya mapambano ya bunduki katika mji mkuu, Niamey. Miezi michache iliyopita Tandja alibadilisha katiba kinyume cha sheria ili ajiruhusu kuongoza kwa muhula wa tatu katika kile ambacho kilionekana kama dhuluma ya halaiki kwenye kura maoni. Wanablogu wanatoa mitazamo yao juu ya maendeleo haya mapya.
Guinea: Jaribio la Kumuua Kiongozi wa Kijeshi Dadis Camara
Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari, Kapteni Dadis Camara, kiongozi wa kikundi cha jeshi kilitwaa madaraka nchini Guinea mwezi Disemba 2008, alipigwa risasi na kujeruhiwa na mmoja wa wasaidizi wake jana mjini Conakry. Wasomaji wengi wa RFI wanaodai kuwa Camara anawajibika kwa mauaji ya waandamanaji wa upinzani yaliyotokea tarehe 28 Septemba, wanaoana kuwa haki imetendeka.