Habari kuhusu Angola
Angola: Raia Wadai Kampeni za Uchaguzi za Wazi
Asasi za kiraia nchini Angola zinatoa wito wa uwazi zaidi [pt] katika maandalizi ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika tarehe 31 agosti, 2012. Moja wapo ya miradi iliyozinduliwa hivi karibuni kwa lengo hilo ni maombi ya mtandaoni [pt] ikiwataka viongozi wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo kushiriki midahalo ya moja kwa moja kupitia...
Afrika: Kusherehekea Siku ya Ukombozi wa Afrika kwenye Mtandao wa Twita
Siku ya Ukombozi wa Afrika ni maadhimisho ya kila mwaka kukumbuka tarehe 25 Mei 1963 siku ambayo Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) ulianzishwa. Mwaka 2002 OAU ilianzisha mrithi wake aitwaye AU. Waafrika na marafiki wa Afrika wanasherehekea siku hiyo kupitia mtandao wa twita.
Angola: Hapo Zamani za Kale Katika Roque Santeiro
Maendeleo yanayoukumba mji wa Luanda unaliwajibisha moja ya eneo la biashara linalotembelewa zaidi mjini humo, eneo ambalo hutengeneza maelfu ya dola kwa siku. Soko la Roque Santeiro limo mbioni kufunga "milango" yake na kufunguliwa katika eneo la kisasa na lenye hadhi, huko Sambizanga.
Misri: Sisi Ni Washindi
Timu ya kandanda ya Misri iliifunga Ghana katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, na ikapata ushindi wake kwa mara ya tatu mfululizo. Huu pia ni ushindi wa saba tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo kwenye miaka ya hamsini. Wanablogu wanaungana na wananchi wa nchi hiyo kusherehekea mafanikio hayo.
Angola: Kombe La Mataifa ya Afrika Moja Kwa Moja Kwenye Mtandao
Pata habari za Kombe la Mataifa ya Afrika yanayofanyika nchini Angola moja kwa moja: “Kwa wale ambao wangependa kuangalia Kombe la Mataifa ya Afrika 2010 kwenye mtandao, kutakuwa na tovuti za michezo zinazotoa mtiririko wa mapambano ya mpira moja kwa moja mtandaoni, bure.”
Angola: Gharama za Juu za Maisha Mjini Luanda
Gharama kubwa ya maisha nchini haieleweki: viashiria vya maendeleo vya hali ya juu havishabihiani na hali ya kifedha ya Waangola wengi na havitafsiriki katika viwango vya maisha vya wasio na hali nzuri kiuchumi.
Angola: Ebola Inapokaribia, Mipaka yafungwa
Baada ya kuzuka kwa ugonjwa wa ebola kwenye Jamburi ya Kidemokrasi ya Kongo, maambukizi ya ugonjwa huo bado hayajafika nchini Angola. Ili kuuzuia kusambaa kwa virusi hatari vya ugonjwa huo, nchi hiyo jirani imefunga mpaka wake na Jamhuri ya Kidemorasi ya Kongo, kadhalika imezuia uhamiaji wa watu kati ya nchi hizo mbili. Anaandika Clara Onofre.
Angola: MPLA Yashinda Zaidi Ya Asilimia 80 Ya Kura na Kutwaa Viti 191
Tume ya taifa ya Uchaguzi nchini Angola imetoa matokeo ya mwisho ya Uchaguzi wa kwanza wa kitaifa katika miaka 16 na imethibitisha ushindi wa chama tawala, Chama Maarufu kwa Ajili ya Ukombozi wa Angola ambacho kimeshinda viti 191 katika ya viti 220 vya bunge. Angalia baadhi ya maoni.
Angola: Uchaguzi Katika Picha
Waangola wako katika uchaguzi kwa mara ya kwanza katika miaka 16 - uchaguzi bado unaendelea Jumamosi hii katika vituo 320 jijini Luanda. Mpaka sasa, hakuna matukio yoyote yaliyoripotiwa, na moyo wa utu umedumu, kama ilivyoangaliwa na mpiga picha Jose Manuel da Silva.
Angola, Brazil: Mshituko na Utengano wa Kitamaduni
Mahusiano maalum kati ya Angola na Brazili yanamaanisha kwamba biashara kati ya makoloni haya mawili ya zamani ya Ureno inashamiri - kadhalika uhamiaji kutoka pande zote za Atlantiki. Lakini, ni vipi hawa watoto wawili wanavyoishi? Ujumbe huu unatoa mitazamo ya wote, kutoka kwa bloga wa Kiangola na wa Kibrazili waishio Luanda.