· Februari, 2009

Habari kuhusu Marekani kutoka Februari, 2009

Clinton Azuru Indonesia

Pamoja na kukutana na viongozi wa Indonesia, Katibu wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton alipata muda wa kutembelea makazi ya watu masikini mjini Jakarta. Kadhalika alitokea kwenye kipindi cha televisheni cha vijana. Ni nini maoni ya wanablogu?

26 Februari 2009

Misri: Wanablogu Wafuatilia Milipuko ya Mabomu Mjini Kairo

Mtalii wa Kifaransa ameuwawa na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya msikiti wa Al Hussein uliopo katika eneo la utalii la Khan Al Khalili mjini Kairo. Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.

26 Februari 2009

Haiti: Fanmi Lavalas na Uchaguzi Ujao

Mwishoni mwa juma lililopita, ulimwengu wa wanablogu wa Kihaiti ulijaa habari za kutengwa kwa vyama vya siasa na Tume ya Muda ya Uchaguzi kwenye uchaguzi wa maseneta utakaofanyika mwezi Aprili 2009 , na siku ya tarehe 6 Januari, tume hiyo CEP ilichapisha orodha ya wagombea ubunge watakaokwaana kwenye uchaguzi ujao wa bunge nchini Haiti. Wanablogu wanaandika mawazo yao kuhusu wagombea walioachwa.

15 Februari 2009