Habari kuhusu Syria

Ukuta Wetu wa Berlin Nchini Syria

  12 Machi 2014

"Wanafunzi wa Syria kwa mustakabali bora" ni blogu ya wnafunzi wa Syria wanaofadhiliwa, ambao wanaitumia kujadili matumaini yao, kukumbuka nyumbani, wasiwasi, mashaka, mitazamo chanya na matumaini kwa Syria iliyo bora.

Video: Usambazaji Vyakula katika Kambi ya Yarmouk-Syria

  5 Machi 2014

Shirika la habari la FAJER liliweka mtandaoni video ya kambi ya wakimbizi ya Yarmouk mjini Damascus wakati wa kupokea mgawo wa chakula cha kuwalisha wakazi 18,000 wa kambi waliobaki, ambao wamelazimishwa kula wanyama waliopotea ili kuokoa maisha yao wakati huu ambapo kuna uhaba mkubwa wa chakula. Video ni ya tarehe...

Pakistan, Usiingilie Vita vya Ndani ya Syria

  27 Februari 2014

Siku moja baada ya dondoo ndogo ya habari yenye kichwa cha habari, “Saudi Arabia ‘inatafuta uungwaji mkono kwa waasi wa” ilipoonekana kwenye magazeti ya Pakistani, mwanablogu wa siasa Ahsan Butt aliposti tahadhari kali kwa watunga sera ya mambo ya Kimataifa wa nchi ya Pakstani kuachana na mambo ya ndani ya...

Syria: Kutwiti Kutokea Vitani Jijini Aleppo

  13 Aprili 2013

Mwandishi wa Habari Jenan Moussa amerudi mjini Aleppo, nchini Syria, akitwiti tajiriba yake wakati vita kati ya vikosi vinavyopinga serikali na vile vinavyoiunga mkono serikali inavyozidi kushika kasi. Twiti za Moussa ni za kawaida na za kibinafsi sana, zikiwapa wasomaji wake taswira ya maisha yalivyo kwa wale walio kwenye uwanja wa vita.

Hali ya Hatari kwa Watoto nchini Syria: Namna Utakavyo Saidia.

  12 Februari 2013

Hadi sasa,inakadiriwa watoto 4,355 wameshauawa katika mgogoro unaoendelea hivi sasa nchini Syria. Mapema wiki hii, tulitoa taarifa juu ya madhila wanayokabiliana nayo watoto wa Syria kufuatia vita hii inayoisambaratisha nchi yao vipande vipande. Leo tunaangalia namna ambavyo watu wanaweza kusaidia kukabiliana na baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo.

Assad atumia Ndege ya Kivita Kuwaua Raia Wake

  28 Disemba 2012

Serikali ya Syria imefanya shambulizi kubwa la angani dhidi ya raia wa nchi hiyo -waliokuwa wamesimama kwenye foleni waisubiri mikate kwenye kiwanda cha kuokea miakte huko Halfaya, Hama. Inakadiriwa kwamba watu waliouawa katika shambulio hilo mjini humo ni kati ya 90 na 300, waasi wakisema kuwa watu hao walikuwa wamejitenga na vikosi vya Assad. Mtandaoni, wanaharakati wanashangazwa inakuwaje dunia inaendelea kutazama tu maisha ya watu wasio na hatia wakiuawa kwa mamia.

Uharibifu Nchini Syria Katika Picha

  27 Novemba 2012

Wapiga picha wa Syria wanatumia mitandao ya kijamii kuweka taswira ya uharibifu katika maeneo mbalimbali na kwenye mitaa. Pamoja na ufinyu wa vitendea kazi vya utoaji wa habari, habari zinazotoka Syria zinaonesha hali ya kutisha ya uharibifu inayoikabili nchi ya Syria.