Habari kuhusu Lebanon

Lebanon: wanablogu washinikiza jarida la Daily Star kubadilika

Wanablogu wa Lebanon wanapiga kampeni ya kwenye mtandao ili kulishinikiza gazeti pekee la kwenye wavuti kurekebisha tovuti yake. Mwanablogu mmoja amefanya jitihada kubuni tovuti ya kuiga - ambayo wenzake wanatumaini itahimiza mabadiliko katika gazeti la Daily Star, na kuibadili 'boti moshi ya Kirusi ya miaka ya 1920' kuwa meli ya karne ya 21 ya abiria.

27 Februari 2010

Tajiri Wa Kimisri Ahukumiwa Kifo

Wamisri walishuhudia hukumu isiyotarajiwa katika historia ya vyombo vya sheria nchini humo: Bilionea Hesham Talaat Moustafa, pamoja na mamluki wake (mpiga risasi wa kukodi) Mohsen El Sokari wamehukumiwa adhabu ya kifo kutokana na kuhusika kwao katika mauaji ya mwimbaji wa Kilebanoni Suzanne Tameem. Mauaji hayo ya kinyama yalitokea huko Dubai, UAE, na hukumu iliyotolewa Alhamisi imesababisha mshtuko na mshangao wakati wanablogu walipojaribu kukubaliana na yaliyotukia.

27 Mei 2009