Habari kuhusu Misri kutoka Februari, 2010
Misri: Mwanablogu apoteza kazi kwa kufichua ukweli kuhusu habari ya bikra za bandia
Mwanablogu ambaye pia ni mwanahabari wa Kimisri Amira Al Tahawi amefukuzwa kazi kwa kufichua ukweli kuhusu habari ya uongo juu ya bikra za bandia zinazotengenezwa China katika makala alioyoichapa kwenye yake, ndivyo wanavyodai wanablogu. Yafuatayo ni baadhi ya maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu za Kimisri kuhusu kisa hicho.
Misri: Sisi Ni Washindi
Timu ya kandanda ya Misri iliifunga Ghana katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, na ikapata ushindi wake kwa mara ya tatu mfululizo. Huu pia ni ushindi wa saba tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo kwenye miaka ya hamsini. Wanablogu wanaungana na wananchi wa nchi hiyo kusherehekea mafanikio hayo.