Habari kuhusu Bahrain

Mwaka Mpya na Mienendo ya Zamani Nchini Bahrain

  8 Januari 2013

Wakati nchi mbalimbali ulimwenguni kote zikiukaribisha mwaka mpya kwa fataki na shamrashamra, serikali ya Bahraini iliandaa utaratibu wa aina yake kwa waandamanaji nchini humo. kwa bahati, watumiaji wa mtandao wa intaneti walikuwa tayari, kuonesha na kuweka kumbukumbu ya baadhi ya matukio kwa ajili ya kushuhudiwa na sehemu nyingine yote ya ulimwengu.

Hakuna Usalama kwa Waandishi wa Kiraia Nchini Bahrain

  1 Januari 2013

Baada ya video ya "kibao" cha polisi wa Bahrain kusambaa sana mtandaoni, Waziri wa Mambo ya Ndani alitoa tamko akiomba kuwa yeyote aliyepiga picha tukio hilo aliripoti haraka kwa mamlaka zinazohusika. Siku mbili baadae, na kinyume na kauli hiyo, watu wengi walishangazwa na kukamatwa kwa mpiga picha.

Uarabuni: Sera ya Romney kwa Mashariki ya Kati Yaibua Mjadala

  8 Oktoba 2012

Hotuba ya Mgombea urais wa Marekani kupitia chama cha Republican Bw. Mitt Romney iliyoelezea sera yake ya nje imeibua mjadala mzito miongoni mwa raia wa mtandaoni leo hasa wale watokao katika nchi za ki-Arabuni. Twiti zinazohoji sera ya mambo ya nje ya Marekani kwa Mashariki ya Kati ziliendelea wakati ambao Romney, anayepeperusha bendera ya chama cha Republican, alipozungumza katika Chuo cha Jeshi cha Virginia. Endapo atachaguliwa, Romney ameahidi kuwa na sera rafiki za mambo ya nje, tofauti na mwelekeo usiotabirika wa sera za Obama wakati huu ambapo mabadiliko ya kisiasa yanaendelea kulikumba eneo la Mashariki ya Kati.

Makala za Global Voices Zilizosomwa Zaidi mwaka 2011

Global Voices haijabaki kuwa sauti pweke ya vyombo vya habari vya kiraia linapokuja suala la twita zinazotuma taarifa na posti za kwenye blogu. Bado, hata hivyo pale ambapo shauku kwa vyombo vikuu vya habari ikindelea kupungua, sisi ndio tunaojibidiisha kuendelea kuweka kumbukumbu ya kile ambacho wanablogu wadogo popote pale waliko wanahitaji dunia ikifahamu. Fahamu orodha ya makala zetu 20 zilizosomwa zaidi kwa mwaka 2011

Bahrain: Waandishi wa Habari Wazuiwa Kuingia Wakiwa Uwanja wa Ndege

  9 Aprili 2011

Bahrain iliingia kwenye vurugu kubwa zilizoambatana na polisi kutumia nguvu dhidi ya waandamanaji waliopiga kambi katika eneo muhimu la wazi linalohusudiwa sana liitwalo Lulu Jumatano iliyopita. Mchana wa siku hiyo nilipanda ndege inayotoka Doha, nchini Qatar, kwenda Bahrain, kwa upande mmoja nikitaka kujionea mwenyewe nini kilikuwa kikitokea katika nchi hii ya kisiwa ambayo ilipata kuwa nyumbani kwangu. Saa kadhaa baadaye nilijikuta kwenye ndege ya kurudi Doha, baada ya kunyimwa ruhusa ya kupita pale uwanja wa ndege.

Twita Kutoka Beirut: Siku ya Pili ya Warsha ya Wanablogu wa Uarabuni

  12 Disemba 2009

Siku ya pili ya Warsha ya Wanablogu wa Kiarabu ilianza na mada inayohusu Mtandao wa Herdict, tovuti inayotumia vyanzo vya watumiaji kukusanya taarifa za uchujaji wa habari kwenye intaneti kutoka kwa watumiaji duniani kote. Mshiriki wa warsha kutoka Qatar Muhammad Basheer alituma picha kutoka kwenye mada hiyo katika ujumbe wa...