Habari kuhusu Chile
Video: Tetemeko la Ardhi Chile Kwa Kupitia Macho ya Raia
Wakati siku inakaribia kuisha, video zaidi za tetemeko la ukubwa wa 8.8 ambalo liliikumba Chile majira ya saa 9.30 usiku zinajitokeza. Tetemeko hilo, ambalo halikuathiri maeneo ya bara pekee kwa njia ya kusogea sogea kwa ardhi, kadhalika lilisababisha mawimbi ya tsunami mabyo yalizua tahadhari katika eneo zima la Pasifiki huku mataifa mbalimbali yakijiandaa kwa mawimbi hayo pindi yatakapofika kwenye fukwe zao.
Chile: Tetemeko Kubwa la Ardhi lenye Ukubwa wa 8.8 Laikumba Chile
Saa 9:34 usiku kwa saa za Chile, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.8 liliukumba mwambao wa eneo la Maule nchini Chile. Tetemeko hilo liliutetemesha mji mkuu wa Santiago uliopo Kilomita 325 kutoka katika kiini cha tetemeko hilo. Uharibifu mkubwa umeripotiwa nchin nzima, na idadi ya waliofariki inazidi kwenda juu.
Amerika ya Kati: Kasi Kubwa ya Ueneaji wa Jangwa
Ueneaji wa jangwa unasambaa kimyakimya lakini kwa kasi kubwa mahali pengi duniani na Amerika ya Kati haijaweza kukwepa hali hii iliyo na athari mbaya za kutisha. Wakati ambapo majangwa ni maumbo ya asili, ueneaji wa jangwa ni mchakato wa kuharibika kwa nyanda za ardhi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na uharibifu unaofanywa na binadamu.
Chile: Mkutano wa McCain na Pinochet Mwaka 1985
Mwaka 1985, Mbunge wa bunge la Marekani aitwaye John Mccain alizuru nchini Chile na kukutana na mtawala wa kiimla Augusto Pinochet, akiwa na viongozi wengine wa serikali. Mkutano huo ambao haujawahi kuripotiwa hapo awali umewekwa wazi na mwandishi wa habari John Dinges, ambaye amechapisha habari hiyo kwenye blogu yake CIPHER [es], kadhalika katika blogu ya Huffington Post, ambako huwa anaandika masuala yanayomhusu John McCain "ambaye amekuwa akishutumu vikali dhana ya kuketi na watawala wa kiimla bila ya masharti yoyote, inaonekana kuwa alifanya jambo hilo hilo analolipinga.