Habari kuhusu Korea Kusini
South Korea: Ahadi ya Rais ya Ustawi Iliyoshindwa Yakosolewa
Rais Park yuko kwenye wakati mgumu kwa r ahadi yake aliyoitoa wakati wa kampeni kuwa angepandisha ruzuku ya pensheni gharama za mafunzo. Wakosoaji wanasema kampeni yake iliahidi kinyume na sera yake kama mgombea mhafidhina, ilimsaidia kuzoa kura katika uchaguzi uliopita. Akaunti ya mtandao wa twita wa @metempirics ilikusanya viunganishi vinavyohusika na...
Korea Kusini: Mpango wa Kuwakutanisha Wenzi Wakwama
Mpango mpya kabisa wa kuwakutanisha wenzi kwa njia rahisi katika mkesha wa Krismas nchini Korea Kusini hatimaye ulijikuta ukishindwa kabisa baada ya waliojitokeza asilimia 90 kuwa ni wanaume. Inasemekana zaidi ya watu 20,000 walijiandikisha na hata polisi walikuwepo kufuatia uwezekano wa vitendo vya ngono za kulazimisha. Mtumiaji mmoja wa mtandaoalibainisha [ko]...
Korea ya Kusini: Mabadiliko ya Sheria kuhusu Uzazi wa Mpango Yaibua Mjadala Mkali
Mamlaka ya Chakula na Dawa ya nchini Korea imetangaza kwamba dawa za kuzuia mimba za dharura zinazofahamika kama 'morning-after pills' zitaanza kupatikana kwa wingi. Hata hivyo, dawa za kuzuia mimba zisizo za dharura zimekuwa dawa za kuandikwa na daktari. Mabadiliko haya ya ghafla kuhusu dawa za kuzuia kuzaliana limeibua mjadala mkubwa mtandaoni.
Korea Kusini: Wahudumu wa ndege wapigania haki ya kuvaa suruali
Katika Siku ya Wanawake Duniani, wahudumu wa moja ya mashirika makubwa ya ndege nchini Korea Kusini, waliitisha mkutano na waandishi wa habari mbele ya makao makuu ya shirika lao la ndege kudai haki ya kuvaa suruali. Madai hayo yamepata uungwaji mkono mkubwa sana na watumiaji wa mtandao wa nchini humo.
Korea Kusini: Dikteta Kim Jong Il wa Korea ya Kaskazini afariki dunia
Kim Jong Il, dikteta wa Korea Kaskazini amefariki. Japokuwa kifo cha dikteta huyo mwenye sifa mbaya duniani ni jambo ambalo watu wanapaswa kulipokea vyema, watu wengi wa Korea Kusini wameonyesha wasiwasi juu ya hali tete katika bahari ya Korea itakayotokana na kifo chake cha ghafla.
Korea Kusini: Maombolezo ya Kitaifa ya Mwanamwali wa Kivietnam
Mwanamwali mdogo wa Kivietnam aliuwawa na mumewe wa Kikorea nchini Korea. Wanablogu wa Korea wanatoa rambirambi zao kwa kifo kibaya cha mke huyo mwenye umri mdogo huku wakiitaka serikali kutokomeza eneo hili lisiloonekana kwa urahisi la haki za binaadamu, linalohusiana na wachumba kutoka nchi za kigeni.
Korea: Ziara ya Clinton Korea Kaskazini
Habari ya kushangaza. Kwa ghafla, Clinton alizuru Korea ya Kaskazini na kama vile 007 aliwarudisha nyumbani wanahabari wawili wa kike ambao walikuwa wameshikiliwa nchini Korea Kaskazini. Kuhusiana na habari hii ya ghafla, hakuna habari zilizowekwa kwenye vyombo vya habari vya umma vya Korea na hata kwenye maoni ya wanablogu. Zifuatazo...
Korea: Wajibu wa Kitaifa Wachuana na Dhamiri
Kijana mmoja anayetumikia jeshi kama askari polisi aliamua kutorudi kwenye kikosi alichokuwa akifanya kazi baada ya likizo na alipeleka taarifa kuwa dhamiri yake ilikuwa ikimshtaki. Sababu ilikuwa kwamba dhamiri yake ilimshtaki baada ya kuwa amewanyanyasa raia walioshiriki katika mkesha wa tukio la kuwasha mishumaa. Uamuzi wa kijana huyu umevuta hisia...